Monday, March 31, 2008

Msaada Kwa Watoto Hawa >>>>


Pichani ni watoto wadogo ambao vichwa vyao ni vidogo kupindukia kwa
mujibu wa mdau Mpoki Bukuku aliyenishushia habari hii hivi punde.
Mama Sophia Lipeleta mkazi wa Nachingwea Mtwara akiwa na watoto wake walemavu pichani na kueleza kuwa alikuwa na watoto saba wa aina hiyo sasa wamebaki hawa watatu baada ya wengine kufa.

Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida.
-------
Wadau kwa niaba ya mdau Mpoki Bukuku aliyeniletea habari hiii hivi punde ni kwamba
kuna watoto wa ajabu wamezaliwa kama muonavyo pichani ambao ni wa Bi Sophia Lipeleta mkazi wa Nachingwea Mtwara ambaye alifika ofisi za gazeti la mwananchi hivi punde kwa nia ya kuomba msaada kwa wasamaria wema kwani watoto wake hawa hawawezi kuongea japokua wana umri mkubwa na kuomba kama kuna mtu atapenda kufanya utafiti anaweza kuwafanyia na kujua tatizo, lakini wako Dar na hawana chakula wala pa kulala kwani hivi sasa wanalala stendi za mabasi. Mama yao anaomba msaada wa hali na mali,nami nimeona niungane na ndugu yangu Mpoki Bukuku kuomba msaada kwa wasamaria wema ili tuwasaidie watoto hawa.
Kwa wale wenye nia ya kuchangia watoto Hawa Mnaweza
kumpigia Simu Mpoki Bukuku kupitia Number hiii
+255222450878 au Fax +255222450886
E-mail:mpokibukuku@yahoo.co.uk

Ndio Maana Naipenda Bagamoyo!


Bagamoyo jana alasiri. Pichani ni hotel ya Millenium.

Ufukwe wake umetulia. Pichani ni jana Jumapili mchana. Mpaka mwisho wa upeo wa macho yako humwoni mtu. Kutoka hapa unaweza kutembea kwa miguu kufuata ufukwe hadi kijiji cha Kaole, huko kuna magofu ya kale. Bagamoyo ni mahali pazuri, gharama zake ni za chini ukilinganisha na sehemu nyingine za kitalii. Ukiwa na shilingi elfu tatu mfukoni Bagamoyo utapata chai ya asubuhi, chakula cha mchana na cha jioni. Na bado utafika beach kuogelea na kupunga upepo. Kutoka Dar hadi Bagamoyo unaweza kufika kwa Daladala, nauli haizidi elfu na mia tano.

Hitimisho...


Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete akitazama muda kabla ya kufunga rasmi
kikao cha halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi (CCM) kilichofanyika Butiama kwa siku mbili na kumalizika jana.kabla ya kufunga kikao hicho Rais kikwete alifafanua zaidi sababu za kufanyika Butiama na alikiri kuwa, kingefanya maamuzi mazito ambayo hayatahusu mageuzi ya kisera wala kiitikadi.Nalisema hili kwa sababu wapo watu wanaotumaini au wenye hofu kuwa hapa Butiama, kutatokea tamko la kurudia tena kutaifisha mali na kuziweka njia kuu za uchumi mikononi mwa dola. Wapo pia wanaodhani tutatoa tamko la kulirudisha nyuma gurudumu la mageuzi ya kisiasa yaliyoleta demokrasia ya vyama vingi na uhuru mkubwa wa watu kutoa maoni yao," alisema.
Kikwete alifafanua kuwa, kikao hicho kingetatafakari hali ya kisiasa, kiuchumi na kiusalama katika chama na taifa na kuwa katika kuzungumzia mambo hayo, yapo masuala makubwa yatakayojitokeza na kufanyiwa maamuzi.

Tumetoka Mbali: Sokoni Kariakoo 1989


Kushoto ni soko mjinga. Samahani picha hiyo imebidi niifute vumbi la kwenye boksi kama inavyoonekana.

Taarifa kwa Vyombo vya Habari !

***Fomu za tuzo za Vinara Zatolewa
---------
Fomu za ushiriki katika kinyang'anyiro cha kuwania Tuzo za Vinara wafilamu Tanzania 2007/8 zimeanza rasmi kutolewa jana katika vituombalimbali nchini ikiwa ni hatua ya kwanza kabla ya kutolewa kwa tuzohizo.Tuzo hizo zitakazotolewa kwa mara ya kwanza nchini, zimeandaliwa nakampuni ya One Game Promotions na kudhaminiwa na Kampuni ya BiaTanzania (TBL) kupitia bia yake ya dovu Power Malt.
Mratibu tuzo hizo, Khadija Khalili, amesema kuwa, kutokana na sababuzilizo nje ya uwezo wao, fomu hizo zilichelewa kutoka kwa tarehe yaawali hivyo kusababisha kuongezwa kwa muda wa kurejeshwa fomu nakupokea filamu zitakazoshiriki katika tuzo hizo hadi Aprili 18 badalaya Machi 31 kama ilivyotangazwa awali.Alisema watengenezaji wa filamu nchini wanakaribishwa kutuma nakala zafilamu zilizotengenezwa kati ya Januari 2007 hadi Machi 31, 2008, kwaajili ya kuwania tuzo hizo.
Khalili alisema kuwa, jopo la majaji litakutana baada ya Aprili 18kuchagua watakaowania tuzo za Vinara wa Filamu Tanzania 2008.Alisema fomu za kushiriki kuwania tuzo hizo zinapatikana katika vituovilivyotangazwa awali ambavyo ni ofisi za Baraza la Sanaa la Taifa(BASATA) kwa Omari Mayanga, pia zinapatikana kwa wasambazaji wa filamuambao ni Wananchi Wote, GMC, Kapico na Game First Quality."Fomu zilizojazwa na nakala ya filamu iliyopo kwenye mfumo wa VCD naDVD zitumwe kwenye ofisi za BASATA zilizopo Ilala Bungoni jijini Dares Salaam au ofisi ya One Game Promotion," alisema.
Vipengele vitavyoangaliwa na majaji katika filamu hizo kuwa ni FilamuBora ya Mwaka, Muigizaji Bora wa Mwaka wa Kiume, Muigizaji Bora waMwaka wa Kike, Muigizaji Bora Chipukizi wa Mwaka wa Kiume, MuigizajiBora Chipukizi wa Mwaka wa Kike, Mwongozaji Sinema Bora wa Mwaka,Mchekeshaji Bora wa Mwaka, Mwandishi Bora wa Filamu, Mtunzi Bora waFilamu, Filamu Bora ya kutisha, Muigizaji Mwandamizii Bora wa kike(supporting actor), Muigizaji Bora Mwandamizi wa Kike, Adui Borakwenye Filamu, Wimbo Bora wa Mwaka (Sound Track), Mhariri Bora waFilamu ambao wote watapata tuzo na zawadi.Pia itatolewa tuzo yaheshima kwa wale waliotoa machango wao kukuza sanaa nchini

Makontena ya mbao kwenda China

WIZARA ya Mali Asili na Utalii imezuia shehena ya makontena kumi ya mbao katika Bandari ya Dar es Salaam ambazo zilikuwa zisafirishwe China baada ya wizara hiyo kuyatilia mashaka makontena hayo.
Sambamba na kuzuia shehena hiyo ya mbao, wizara hiyo inamchunguza afisa wa wake aliyekagua na kuidhinisha mbao hizo, ili zisafirishwe licha ya kuwepo kwa aina mbalimbali za mbao. Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Waziri wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwangunga alisema makontena hayo yamezuiliwa baada ya kubaini kuwa kuna udanganyifu uliofanywa na mfanyabiashara mmoja ambaye hakumtaja jina kwa kuwa uchunguzi bado unaendelea,Habari hii na James Magai.

Tamwa..


Mke wa Rais Salma Kikwete, akikata utepe kufungua rasmi jengo la Makao Makuu ya Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) lililoko Sinza Mori Jjijini Dar es Salaam jana.Uzinduzi wa jengo hilo ni sehemu ya maadhimisho ya miaka ishirini ya TAMWA

Mzegamzega!


Picha hii niliipiga Bagamoyo mwaka juzi.

KP LEO !!

William Ngeleja akizungumza na maafisa wa kampuni ya Tanzanite One


Waziri wa Nishati na Madini ,William Ngeleja akizungumza na maafisa wa kampuni ya Tanzanite One, Zane Swanepoel, yaani umbali wa machimbo haya sio mkubwa nashangaa kwa nini hawajaingia kusaidia watanzania waliopata maafa mpaka wafuatwe na mawaziri. Ndio maana wanaapollo wana hasira nao sana, inabidi wabadilike vinginevyo........!!!!!!!!!

Waziri wa mambo ya Ndani, Lawrence Masha akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Tanzanite One, Zane Swaanepoel na afisa toka kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Barrick ili kuanza mikakati ya kuopolewa miili ya wachimbaji wadogo jana Mererani.

Askari wa kikosi cha FFU akiwa anawalinda wachimbaji wadogo ambao walikuwa wanazungumza na mawaziri waliotembelea Mererani kutaza maafa. Hawa jamaa kama wakiletewa ujinga hawasikii vibaya kulianzisha zali.

MSAFIRI KAFIRI !!


Jamani mimi nashindwa kuelewa ndugu zetu wa Mbagala, Dar es Salaam yaani wamezoea kugombea mabasi hata wakiwa watatu kituoni watapitia dirishani. mazoea haya yamewafanya hata kwenye lift wanagombea kuingia.

BODABODA IN DAR?


Jamaa wa kidosi akiwa amepakia abiria wake kwenye pikipiki katika moja ya mitaa ya Dar es Salaam, sijui kama alifika salama bila kupigwa 'bao'.

Kumbukumbu kutoka kwa Mzee Wa Sumo Mererani !!


Hapa ndio mbali na duniani chini ya shimo baada ya washikaji kufa nimekumbuka nilienda kama 450m underground kupata picha hizi lakini washkaji wote wako shwari.

Jamaa huyu wa mbele nilimwadikia makala anaitwa Kambi (Macharii wa AR watakuwa wanamfahamu) aliwahi kupata jiwe( Tanzanite) ikatisha! Alikuwa anakodi ndege kwa siku kadhaa kuzunguka sehemu mbalimbali sasa hivi karudi tena shimoni kuangalia kama atapata tena.

Hapa ndio Mzee wa Sumo anarejea kutoka Sobiboh camp chini ya ardhi wenyewe kama hapa wanasema ndio mtu unarudi duniani.

(Mzee Wa Sumo anaendelea kulonga)Kwa Kusema Tuache utani huko chini kama maji yamekuja hakuna kupona cheki nilivyokuwa hoi hata Konyagi haikupanda kwa siku mbili ningebaki huko nundu hiii ingeondoka tumboni!

KIAPO CHA WAZIRI Wetu John !!


MIMI JOHN LAGER MAGUFULI, NAAHIDI KUTOIRICHMOND NCHI YANGU NA KWAMBA NITAMWAKYEMBE MTU YEYOTE ATAYEIBALALI NCHI YANGU.

NITAJIEPUSHA NA UNGOYAYI, UKARAMAGI, AU USABAHA WA AINA YEYOTE NA KWAMBA WAKATI WOTE NITAWALINDA WOTE WANAOISLAA, AU KUIZITO NA KUIKILANGO NCHI YETU.

EWE MWENYEZI MUNGU NIBARIKI.

Ndio maneno ya mdau JAMANI NAUZA.........


Sifa za hiyo simu ni kama zifuatazo na haya maneno sio yangu bali ni ya mdau alionitumia kumtafutia wateja katika blog yetu inayokuwa kwa kasi ya ajabu kama moto ule uliounguza jengo la ushirika pale town anaanza kwa kusema mdau KANOKIA KANGU,KAKO NA CAMERA,2MEGA PIXEL,MEMORY CARD,BLUE TOOTH, @ 20,000/=

Nasikia mjamaa anakaribia kushinda tena !!

Saturday, March 29, 2008

TAFAKURI

Kuna mdau mmoja Baraka Karashani kanipa hii:
ANGALIA MZUNGUKO WA SAA YAKO.
Kuna mtu mmoja alifariki dunia na akaenda kwa Mungu,alipofika akakuta saa za ukutani nyingi sana zimetundikwa. Akauliza "Hivi hizi saa ni za nini huku?" Akajibiwa na Askofu mkuu aliyemkuta huko, "Kila saa ina dhambi za kila Binadamu,ikizunguka mara moja ina maana ametenda dhambi mara moja".
Yule jamaa akauliza "mbona hii hapa imesimama ni mbovu? Akaambiwa hiyo ni ya mama Theresa, na inamaanisha kuwa hakutenda dhambi kabisa ndio maana imesimama.
Jamaa ikabidi aulize tena, "hivi saa ya Edward Lowasa na Ballali iko wapi kati ya hizi?" akajibiwa, "ya hao ndugu iko ofisini kwa Bwana Yesu mwenyewe maana anaitumia kama feni kwa jinsi inavyozunguka mara nyingi na kwa kasi."

MATOKEO YA MVUA SASA


Wakazi wa mabibo Dar es Salaam wakikatisha katika daraja lililoshushwa na mvua za juzi mbali na uharibifu majumbani miundombinu nayo haikupona.Watu watano wamefariki dunia, wakiwemo wanne waliofariki kutokana na mvua kubwa iliyonyesha juzi jijini Dar es Salaam.

Wakati mvua hiyo ikuua, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetoa tahadhari kuwa mvua za masika zilizoanza huenda zikaleta madhara zaidi kwa wananchi wanaoishi mabondeni.

Watoto wa watu waliovunjiwa nyumba zao Tabata dampo wakichota amaji ya mvua, sijui ni kutokana na uhaba wa maji ama mchezo tu!

Mgogoro wa maiti: Wakristo, Waislamu sasa kwenda mahakamani

Na Jackson Odoyo

SIKU moja baada ya kutokea vurugu za kugombea maiti kati ya waumini wa dini ya Kikristo na Kiislamu na kisha Jeshi la Polisi kuingilia kati kwa kuchukua maiti hiyo kuirudisha katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Mwananyamala, pande zote mbili zimeamua kwenda makahamani.

Wakizungumza na Mwananchi Jumapili jana kwa nyakati tofauti waumini wa dini hizo wamesema, watakwenda kufungua kesi katika Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu ili kudai haki ya kuuzika mwili huo.

Ibrahimu Msumari ambaye ni Shemeji wa Marehemu, Paul Goriam (40) alisema watakwenda kufungua kesi katika Mahakama ya Kisutu Machi 31 mwaka huu, ili kudai maiti hiyo aliyosema ndio wana haki ya kuizika.

Msumari alisema wao ndio ndugu wa damu wa marehemu, hivyo hakuna shaka yoyote kuhusu hilo na wala hakuna atakaye pinga kwamba marehemu hakuwa ndugu yao.

Alisema sababu nyingine inayowaruhusu kuuzika mwili huo ni kuwa marehemu alikuwa Mkristo safi.

Msumari alisema marehemu alizaliwa katika familia ya wakristo mwaka 1968, akalelewa katika familia hiyo mpaka alipofariki dunia na kwamba, japo mwaka 2004 alibadili dini na kuwa muumini wa dini ya kiislamu lakini bado alikuwa analelewa katika familia hiyo ya wakristo.

Alisema marehemu aliamua kurudi katika dini aliyozaliwa ya kikristo mwaka 2006 na kubatizwa tena kwa kufuata kanuni na taratibu zote za kikristo.

Msumari alisema mara baada ya marehemu kutubu dhambi zake na kuwa Mkristo, aliendelea kutekeleza imani ya dini hiyo.

�Ninashangaa kuona wenzetu wa dini ya kiislamu wanadai kuwa, marehemu alikuwa muumini wao lakini kipindi chote alipoumwa hatukuwaona hata kuja kumletea panado iweje leo hii waseme marehemu alikuwa muumini wao?,�alihoji Msumari.

Naye Imamu wa Msikiti wa Swafa, Othman Njama alisema yeye akiwa kama Imamu wa msikiti aliokuwa anaswali marehemu, ndiye mwenye dhamana ya mwili wa marehemu kuanzia kipindi cha uhai wake hadi mauti yalipompata.

Imamu Njama alisema kutokana na dhamana aliyokabidhiwa kwa mujibu wa misingi ya dini ya kiislamu, wako katika majadiliano kati yake na kamati iliyoundwa kushughulikia suala hilo.

Alisema moja ya majadiliano ambayo wanafanya ni kuamua kesi hiyo ikafunguliwe mahakama gani, japo kulingana na uzito wa kesi wanatarajia kufungua kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Imamu huyo alisema mbali na kufungua kesi hiyo wana imani ya kushinda kesi hiyo kwa sababu mpaka marehemu anafariki dunia alikuwa muumini wa kiislamu katika Msikiti huo wa Swafa na yeye ndiye aliyekuwa Imamu wake.

Yvone Chaka Chaka atua bongo


Mwanamuziki nyota kutoka nchini Afrika Kusini Yvone Chaka Chaka ambaye kwa sasa ameokoka ametua leo mchana jijini dar kwa ajili ya uzinduzi wa albamu mpya ya kundi la New Kitim tim inayaoitwa vita hii yatoka wapi utakaofanyika kwenye ukumbi wa diamond jubilee kesho mchana.Pichani ni Yvone Chaka Chaka akifanya mahojiano na mtangazaji wa televisheni ya Taifa (TBC) mara baada ya kutua uwanja wa ndege wa JK leo mchana

Hata Kaburini, Mwalimu Bado Anatusikitikia


( Pichani Mwalimu akiwa Mbeya mwaka 1963. Wengine ni Kaunda na Kawawa. Picha ya maktaba yangu)

Na Maggid Mjengwa
“KAMA mtaamua fedha kuwa ndio chanzo cha kuwapatia viongozi, basi mjue nchi inakwisha na CCM inakwisha"... ( Mwalimu Nyerere)

Tuta Hilo!

Hi Kaka Safari,


Musaada Kwenye Tuta

Swimmers Wanted
I am putting together competition of swimming from Magogoni to Kigamboni the 1st 2nd 3rd Places winners to get good prizes, which to be determined soon. If you or your organization interested to be part or Sponsors this event please contact me MAGO2KIGA@GMAIL.COM

Kumbukumbu Ya Kifo Cha Moshi William TX


Leo ni siku ya kumbukumbu ya kifo cha mwanamuziki wa msondo ngoma ambaye ambaye alikuwa mtunzi mahiri wa nyimbo na mwimbaji maarufu wa msondo ngoma tx moshi william. Redio Ebony FM ya hapa Iringa itafanya kipindi maalum leo kumkumbuka . Ni miaka miwili sasa tangu afariki tarehe 29 March 2006.

Nyota wa BBS 2008 huyu hapa


Huyu ndio nyota wa bongo star search 2008,Misojo Mkwabi

Mshindi ni Misoji Mkwabi aliyejinyakulia kitita cha milioni 15 pamoja na zawadi nyingine kede kede

Rogger Luca ambaye aliibuka kuwa mshindi wa pili akiimba huku akilikung'uta gitaa lake kuonesha yuko fiti kila idara ila hakufua dafu kwa Msichana Misoji Nkwabi alieibuka mwimbaji mwenye kipaji Tanzania katika onyesho la Bongo Star Search lilikuwa jana usiku kwa Misoji Nkwabi kuwa mshindi aliyejinyakulia kitita cha Sh18milioni na zawadi nyingine kem kem baada ya kuwazidi ujuzi washiriki wengine watano waliofika fainali kwa kupigiwa kura na watazamaji.

Onyesho hilo lilofanyika kwenye ukumbi wa Blue Pearl Ubungo Plaza jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Joel Bendera lilichangamshwa na wanamuziki kutoka Jamaica Brick and Lane walionekana kuzitega nyanyo za wapenzi walijazana kwenye ukumbi huo.

Onyesho hilo lilianza majira ya saa 9:30 usiku huku wasanii wote wakitumbuiza nyimbo mbili mbili mbele ya watazamaji waliokuwa mbele yao na kushangiliwa kwa wingi na umati huo.

Mara baada ya kupigwa kwa nyimbo hizo ambazo kama mazoea kuanzia onyesho hilo lianze miezi saba iliyopita wengi wao wameshindwa kutunga nyimbo zao wenyewe na wamekuwa wakiimba za wasanii wengine, majaji walitoa majina ya washindi kuanzia mshindi wa tano hadi wa kwanza na ndipo Mkwabi alipotangazwa kama mshindi wa kwanza kwa kushindi kitita hicho.

Mbali na Fedha, dada huyo alijinyakulia simu kutoka kampuni ya LG, Sofa seti toka the Living Room, TV, Gomputer, nafasi ya kusoma chuo cha uandishi wa Habari Times, ngazi ya Diploma pamoja na zawadi nyingine kem kem.

BREKING NYUUUZZZZZ

RAINS CLAIM LIVES IN MERERANI
From SUKHDEV CHHATBAR in Arusha
At least 75 miners are missing and believed to have died in mines following Friday’s heavy rains at Mererani, the world’s only producer of Tanzanite, a semi-precious blue-purple stone used by the jewellery industry.
Manyara Regional Commissioner Henry Shekifu says mine owners reported the 75 men went missing Friday as heavy rains pounded their mines in Mererani, 25 miles southeast of Arusha.
Shekifu said that the government was to assess the situation and consider how fast to get equipment to the mines to drain the water in hopes of retrieving the men.
“We want to first take stock of the situation and act swiftly,” he told this reporter, as he was rushing the scene of the accident at Block “B”.
He did not rule out the death toll to be much higher.
”The death rate can be much higher but we can only say that once we have all the information from affected mine pits.”
He said that the rains entered about eight pits and later spread underneath to other mines, drowning miners at work.
Reports from Mererani say that five bodies have already been fished out with the help of miners in the area and volunteers.
The dead identified are: Nelson Mmari(31), Uda Njau(40), Yonas Paul (28) and one person identified by only one name as Mushi. Another person is yet to be identified.
The bodies were rushed to the Mount Meru Hospital in Arusha for preservation and to be collected by their relatives. The area was filled by relatives and miners anxious to know fate of their loved ones.
Suddenly, Mererani normally bubbling with activities was caught in a somber mood. The exercise to fast recover bodies was partly hampered because electric poles were also washed away leaving the area without any electricity.
However, Tanesco engineers were making frantic efforts yesterday to restore electricity so that water pumps can begin to suck out water from the water-filled pits. Some private miners brought their small generators for the exercise but are not enough to speed up the exercise.
More bodies are expected today if the electricity will be restored and equipment brought in timely.
Mererani witnessed one of the worst accident in 1998 when about 100 miners died following the El-nino rains.
In 2002, again 40 lives were lost when miners were trapped inside after an oxygen machine failed

choki na werrason


kiongozi mpya wa bendi ya tot ali choki akiwa na mwanamuziki mahiri wa kongo werrason wakati choki alipokuwa kinshasa kusaka wanamuziki kwa ajili ya bendi yake hivi karibuni. choki amesharejea na wanamuziki takriban wanne na sasa wako kambini wakijifua kabla ya kutoka upya

mnaambiwa bongo tambarare hamsikii

mnaambiwa bongo tambarare hamsikii
Bro Safari,

Napitia uani mzee kwani kupitia mbele inashindikana itabidi labda unielekeze kwa haraka nini nakosea. Inawezekana ni setting kwenye computer yangu. Eee bwana nina issue hapa naomba iwekwe hadharani lakini tumia jina hili MPIGANIA HAKI.

Ninaandika masikitiko yangu kwa TRA Dar es alaam namna wanavyorudisha nyuma jitihada za kuinua uchumi na badala yake wanatengeneza mazingira ya rushwa. Sijui kama tutashinda vita dhidi ya mafisadi.

Nikiwa mwanafunzi huku abroad nimejibana kutuma gari huko nyumbani kwa mzee wangu lisaidie familia. Gari ni isuzu used nimelinunulia Japan kwa gharama nafuu kabisa. Kuepuka usumbufu wa kipengele cha kuingiza gari lisilozidi miaka 10, basi nilinunua gari ya mwaka 1999.
Gari ilisafirishwa toka Japan mwezi wa 11 mwaka jana na kuingia bongo mwishoni mwa desemba 2007. Jamaa zangu huko home walifuatilia kulitoa na jamaa wa TRA wakasema lilipiwe milioni 5 kwa maelezo eti ni la kifahali. Hatukubishana, pesa ilitafutwa ikalipwa.
Nikapata taarifa eti TRA wametupiga faini ya milioni 2 zaidi kwasababu wamegundua gari ni ya mwaka wa nyuma imeandikwa kwenye mikanda tofauti na ilivyoelezwa kwenye papers.
Mimi nikahisi kuna harufu ya dhuruma hivyo nikawaambia ndugu zangu wasilipe fine wafuatilie kiundani. Wakawasiliana na kampuni inayoingiza magari ya isuzu toka Japan. Jamaa wakawapa taarifa ya maandishi kuwa gari used zinazonunuliwa Japan zinafungwa vifaa vipya kuondoa vichakavu.
Kuna uwezekano mkanda uliofungwa ukawa mwaka tofauti na manufacture date ya gari. Barua ilipelekwa TRA kwa wahusika basi mpaka leo Michuzi inapigwa dana dana. Wanasema wiki hii eti kuna sekretari TRA aliipoteza barua haikuweza kuingia kwa mkubwa, hivyo wakahitaji copy ambayo tulikuwa nayo waiingize kwa mkubwa.
Sijui itachukua muda gani na gari iko bandarini muda wote huo.


Nimeona uozo huu niuanike hadharani ili kama kuna yoyote anayeweza kunisaidia anisaidie.

MPIGANIA HAKI

Makamuzi ya Brick & Lace Bongo ..........


Wanamuziki kutoka nchini Jamaica Brick & Lace wakifanya vitu vyao ambao usiku wa jana ndio walikuwa wageni rasmi kwenye mashindano la Bongo Star Search lilofanyika usiku wa jana ndani ya ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam ambapo Misojo Mkwabi aliibuka mshindi wa shindano hilo kwa mwaka 2008.

Madalali 11 waomba kukusanya Fedha !!

KAMPUNI 11 za udalali zimeomba zipewe kazi ya kukusanya Sh bilioni 199 zilizochotwa serikalini na ‘wajanja’ kupitia Mpango wa Uagizaji wa Bidhaa Nje (CIS), lakini zikatumika kwa matumizi mengine bila kurudishwa. Wizara ya Fedha na Uchumi inalazimika kutumia madalali kukusanya fedha hizo kutokana na watu waliochota fedha hizo kwa kisingizio cha kuagiza bidhaa nje kugoma kuzirudisha kama mkataba ulivyowataka kufanya.

Jana ilikuwa siku ya mwisho ya kuwasilisha zabuni za kufanya kazi hiyo ya kukusanya mabilioni hayo ya fedha. Hadi kufikia saa nne jana, kampuni 11 ndizo zilikuwa zimewasilisha maombi ya zabuni hiyo.

Kampuni itakayopewa kazi hiyo italazimika kukusanya madeni hayo kutoka kwa watu na kampuni zipatazo 916 ambazo zilikopeshwa Yeni ya Japan Bilioni 16 (Sh bilioni 199). Watu hao wamegoma kurejesha fedha hizo, kitendo kinachotafsiriwa kuwa ni ufisadi dhidi ya fedha za umma.

Kampuni za udalali zilizoomba kufanya kazi hiyo ni Yono Auction Mart, Majengo Auction Mart, Rhino Auction Mart, Msolopa Investment Co Ltd, Bani Investment Ltd, Kitindi Co Ltd, GM Auction, Mpoki & Associates Advocates, Nakara Auction Mart, Aslyla Attorneys & TMK Enterprises na Rex Attorney. Kila kampuni ambayo imeomba kufanya kazi hiyo imeambatanisha dhamana ya Sh milioni mbili na mapendekezo ya riba inayoombwa ilipwe kutokana na kiasi cha fedha itakachokusanya.

Wizara ya Fedha na Uchumi imeitisha zabuni hiyo huku tayari ikiwa imeshatishia kuwaanika hadharani na kuwachukulia hatua za kisheria watu waliochota fedha hizo kama hawatalipa deni hilo ndani ya miezi mitatu tangu tangazo hilo lianze kutoka kwenye vyombo vya habari.Miongoni mwa wadaiwa hao wamo wafanyabiashara maarufu nchini, wanasiasa wakiwamo wabunge na baadhi ya maofisa wa serikali.Habari hii kwa msaada wa Shadrack Sagati

Waasisi....


Pichani watoto wa viongozi waasisi wa Tanzania kutoka kushoto ni Rais Amani Karume wa zanzibar ,Mtoto wa mwanasiasa mkongwe nchini(simba wa vita) mzee Rashid Kawawa Bi Zainabu Kawawa na Makongoro Nyerere mtoto wa Rais wa kwanza na Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere wakitambulishwa rasmi mjini musoma,Butiama jana..

Mambo Yote Butiama...


Rais jakaya kikwete akiwapungia wananchi wa Butiama kabla ya kuingia kwenye ukumbi wa kumbukumbu ya Joseph Kazurira Nyerere ulioko Butiama kuongoza mkutano wa Kamati kuu ya CCM jana.Kushoto ni katibu mkuu wa CCM, Yusufu Makamba na wapili kushoto ni mkamau mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa.

Rais jakaya Kikwete akisalimiana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ukumbi wa kumbukumbu ya Joseph Kazurira Nyerere, Butiama jana kuongoza mkutano wa Kamati Kuu ya CCM. Wengine pichani kutoka kushoto ni Mama Maria Nyere, katibu Mkuu wa CCM , Yusufu Makamba, Makamu wa Rais, Dr. Ali Mohammed Shein, Makamu Mwenyekiti wa CCM Mstaafu, John Malecela na Waziri Kiongozi wa Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha.
-----------------
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Mrisho Kikwete jana ameongoza kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) katika kijiji cha Butiama, wilaya ya Musoma, Mkoa wa Mara.Kikao hicho kimeanza tu muda siyo mrefu baada ya Rais Kikwete kuwa amewasili Butiama tayari kwa kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM .

Kikao cha NEC kinaanza kesho ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika katika kijiji ambako alizaliwa Baba wa Taifa na mwanzalishi wa taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.Rais Kikwete aliwasili Butiama kwa barabara akitokea Mwanza ambako ndege yake ilitua katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza mapema asubuhi na akaamua kusafiri kwa gari kwenye Musoma.Mjini Mwanza, mamia ya wakazi wa mji huo na vitongoji vyake, walijitokeza kwa wingi, katika baadhi ya sehemu za jiji hilo mvua ikiwa inanyesha, kumshangilia Rais wakati msafara wake ukikatisha mitaa ya jiji hilo kuelekea Musoma.

Friday, March 28, 2008

Mh Zitto Kabwe afichua Siri...


NCHI wahisani zimetishia kutochangia bajeti ya nchi ya mwaka 2008/2009 kama serikali haitachukua hatua kali dhidi ya mafisadi waliochota mabilioni ya shilingi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) na mkataba wa kinyonyaji wa kufua umeme wa dharura kati ya serikali na Kampuni ya kitapeli ya Richmond.
Hayo yalibainishwa jana na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema) wakati akichangia katika kikao cha mwongozo wa kutayarisha mipango na bajeti ya serikali kwa kipindi cha mwaka 2008/2009 kwenye Ukumbi wa DICC, Dar es Salaam, kauli ambayo ilimlazimisha Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo kukiri.

BREAKING NEWS !!

Kwa wasomaji wa blog hii ambao walionyeshwa kukerwa na kitendo cha kondakta wa daladala mjini Dodoma cha kumyanyasa Msichana ambaye ni mwanafunzi wa shule ya secondary Msalato napenda kuwajulisha kuwa kondakta yule amekamatwa na polisi kwa mujibu wa mdau bukuku aliyetwanga picha zile akiwa mjini Dodoma hivi karibunikwa habari zaidi baadae......
*kwa wadau wasiojua waangalie picha zilizopita chini ataona *

Wajumbe wawasili Butiama..


Wajumbe wapatao 22 kutoka chama tawala Tanzania( CCM) wakiweka mataji ya maua katika kaburi la Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, nyumbani kwake Mwitongo, Butiama jana kabla ya kuanza mkutano mkuu wa NEC unaotarajiwa kufanyika kwa siku mbili kuanzia kesho kesho chini ya mwenyewekiti wake Rais Jakaya Kikwete..picha kwa msaadawa mpoki Bukuku.

Makatibu Wakuu.


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw Ban Ki-Moon(kushoto) Naibu Katibu Mkuu wa U mojahuo Dr Asha-Rose Migiro(kati) wakiwa katika picha ya pamoja na katibu mkuu mstaafu wa umoja huo Bw Koffi Annan walipokutana Luncgeon Mjini New York Jana.

ismail aden rage ni mtu huru sasa !!!



MAHAKAMA ya Rufaa jana imemsafisha Rais wa klabu ya Moro United Ismail Aden Rage baada kushinda rufaa ya hukumu iliyotolewa wakati akiwa Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Tanzania (FAT) na sasa TFF miaka sita iliyopita.
Majaji Damian Lubuva, John Mroso na Mbarouk S. Mbarouk wamefuta hukumu ya miaka mitatu jela iliyotolewa mwaka 2005 na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ya jijini Dar es Salaam na baadaye kuthibitishwa na Mahakama Kuu.
Imebainika kuwa hakukuwa na vielelezo vya kutosha kuonyesha kuwa Rage alitenda kosa alilohukumiwa nalo. Wakati wa kusikiliza rufaa hiyo, mwendesha mashitaka alikiri kuwa hatia aliyokutwa nayo Rage kutokana na makosa mawili haikuwa sahihi.
Makosa aliyokuwa akikabiliwa nayo ni yanayomhusisha kuiba Sh milioni 1 kutoka Salvation Army ya jijini Dar es Salaam ambako timu ya Taifa iliweka kambi kwa ajili ya maandalizi na michezo ya kimataifa na Sh 400,000 alizodaiwa kuwalipa posho wachezaji. Habari kamili

kibaka abambwa akitaka kufanya Tukio !!


wananchi wenye hasira wakimsulubu jamaa anayesadikiwa kuwa ni kibaka baada ya mtu aliyetaka kumchomolea pesa mfukoni kumshtukia na kuanza kupambana naye sasa hivi mtaa wa samora avenue.

jamaa wakiendelea kumwadhibu mtuhumiwa huyo huku jamaa aliyepigwa poketi (mtasha, shati bluu) akijisachi

kwa kuogopa shari jamaa aliyetaka kupigwa poketi anaamua yaishe na kuanza mbele akiwaachia wadau wamalizne na kibaka ambaye hatimaye aliachiwa. siku za karibuni vibaka wamekuwa wengi sana maeneo y katikati ya jiji ambako inabidi doria iimarishwe..

KP Leo !!

Thursday, March 27, 2008

HAKI NA USAWA KWA WANAFUNZI !!



Mwanafunzi wa shule ya Sekondari ya Msalato Dodoma akiwa ananyanyaswa na Konda wa daladala akitakiwa alipe nauli ya Sh400 ya mtu mzima! Unayanyasaji huu nilifikiri uko Dar tu!

" Jamani Niliuliza Tu, Kulikoni Refa?"


Javier Mascherano wa Liverpool alichemsha. Kwa mchezaji mzoefu kama yeye hakutakiwa kufanya kama alivyofanya. Kitendo cha kugomea kutoka uwanjani kitamgharimu adhabu zaidi kutoka FA, na aisubiri.

Mgeni Njoo Mwenyeji Apone!


Barabara za mji wa Iringa zimeanza kuwekwa taa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mei Mosi zitakazofanyika kitaifa hapa Iringa na ujio wa Mh. Rais Jakaya Kikwete sambamba na sherehe hizo. Pichani fundi wa TANESCO akifunga taa ya barabarani juzi mchana.

Mvua kubwa yasababisha vifo Jijini Dar es Salaam !!



WATU watano wamefariki dunia, wakiwemo wanne waliofariki kutokana na mvua kubwa iliyonyesha juzi jijini Dar es Salaam.

Wakati mvua hiyo ikuua, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetoa tahadhari kuwa mvua za masika zilizoanza huenda zikaleta madhara zaidi kwa wananchi wanaoishi mabondeni.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Emmanuel Kandihabi alisema, jana saa 10.00 jioni maeneo ya Mbagala Kiburugwa, Saidi Mkumba (75) alifariki dunia kwa kudondokewa na ukuta wa nyumba wakati mvua ikinyesha.

Kandihabi alisema, ukuta uliosababisha kifo hicho ulikuwa wa nyumba ya mtoto wake, Fadhili Lila (32).

Katika tukio la pili, Hadija Shabani (3) alifariki dunia baada ya kudondokewa na ukuta wa nyumba yao maeneo ya Manzese Uzuri.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Jamal Rwambow alisema, juzi saa 1.00 jioni maeneo ya Manzese Uzuri mtoto huyo akiwa anajisaidia pembeni mwa ukuta huo ulianguka na kumuua papo hapo.

Katika tukio lingine, Rwambow alisema, mkazi wa Mikocheni, aliyefahamika kwa jina moja la Mawaya (30) alifariki dunia baada ya kutumbukia kwenye mtaro uliokuwa umejaa maji yaliyotokana na mvua hiyo.

Rwambow alisema, tukio hilo lilitokea saa 3.00 usiku makutano ya barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi na kwamba, Mawaya (30) na Michael Charles (59) wakiwa wanatembea kwa miguu kando ya barabara hiyo, ghafla waliteleza na kutumbukia mtaroni uliojaa maj.

Katika tukio jingine lililosababishwa na mvua hiyo, lilitokea Tandale Sokoni ambako mtoto Rehema Hamis (1), alifariki dunia baada ya kutumbukia kwenye mfereji wa maji,jirani na nyumba yao.

Wakati huo huo, Kaimu Mkurugenzi TMA, Abidan Mlaki alisema, mvua kubwa zinaweza kunyesha katika kipindi kifupi katika baadhi ya maeneo.

Mlaki alitoa mfano wa mvua zilizonyesha juzi jijini Dar es Salaam na Zanzibar, kuwa ni kubwa tofauti na walivyotarajia na kwamba, awali mikoa itatabiriwa kiwango kidogo hadi chini ya wastani ni Dar es Salaam, Tanga, Pwani, Kaskazini mwa Morogoro na visiwa vya Pemba na Unguja.

Pia, Mlaki alisema izingatiwe kuwa mvua za msimu wa Machi hadi Mei ni muhimu zaidi kwa maeneo ya kaskazini mwa nchi na matukio ya vimbunga Bahari ya Hindi.

Alisema mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara mvua zinatarajiwa kunyesha kwa kiwango cha wastani na juu ya wastani.

Bongo jana ilikuwa hamna pakukanyaga !!!






Jamani majengo yanajengwa ila maji taka pakupita hakuna ndio haya yaliyojiri jana mvua ilivyo nyesha sasa hapa wale wakazi wa Tabata Dampo ambao walivunjiwa nyumba zao jana walipona kweli na mafuriko haya kweli !!