Saturday, March 15, 2008

Mabadiliko ya hali ya hewa yameanza kuleta madhara katika bara la Afrika

Wataalam wa masuala ya mazingira wamesema mabadiliko ya hali ya hewa yameanza kuonyesha dalili za kusababisha madhara mbalimbali katika bara la Afrika.

Wakizungumza jijini Dar es Salaam katika mkutano wa kimataifa unaojadili mabadiliko ya hali ya hewa barani Afrika, wataalam wa mazingira, wametaja baadhi ya madhara hayo kuwa ni pamoja na upungufu wa chakula kutokana na ukame.

No comments: