Monday, March 31, 2008

Kumbukumbu kutoka kwa Mzee Wa Sumo Mererani !!


Hapa ndio mbali na duniani chini ya shimo baada ya washikaji kufa nimekumbuka nilienda kama 450m underground kupata picha hizi lakini washkaji wote wako shwari.

Jamaa huyu wa mbele nilimwadikia makala anaitwa Kambi (Macharii wa AR watakuwa wanamfahamu) aliwahi kupata jiwe( Tanzanite) ikatisha! Alikuwa anakodi ndege kwa siku kadhaa kuzunguka sehemu mbalimbali sasa hivi karudi tena shimoni kuangalia kama atapata tena.

Hapa ndio Mzee wa Sumo anarejea kutoka Sobiboh camp chini ya ardhi wenyewe kama hapa wanasema ndio mtu unarudi duniani.

(Mzee Wa Sumo anaendelea kulonga)Kwa Kusema Tuache utani huko chini kama maji yamekuja hakuna kupona cheki nilivyokuwa hoi hata Konyagi haikupanda kwa siku mbili ningebaki huko nundu hiii ingeondoka tumboni!

No comments: