Thursday, January 29, 2009

Ama kweli duniani kuna mambo.!


mkubwa fella aja na singo yake kuleta heshima


Anaitwa Said Fella lakini unaweza ukaanza kumuita kwa jila la Mkubwa Fella nae bila hiyana huitika kwa bashasha kabisa.Kwa wale wasiomfahamu vyema ni yule meneja wa kundi la Wanaume TMK Familly lenye makao yake makuu kule kule Temeke jijini Dar.

Mkubwa Fella amenitonya hivi punde kwa njia ya simu kwamba ameingia studio ya Sound Crafterz kwa ajili ya kurekodi singo yake ya kwanza itakayoitwa 2009.Amesema kuwa anataka kuwaonesha baadhi wasanii ambao wamekuwa wakimfuata wakati wa shida na kusaidiwa, wakishiba wanakuja na maneno ya kashfa na kiburi kama baadhi ya wasanii wengine ambao wamekuwa wakimtuhumu kwa maneno ya hapa na pale.

"Nataka kuwaonesha baadhi wasanii kuwa hata mimi na naweza,ili kuthibitisha hilo wakae mkao wa kula nakuja na singo yangu ya kwanza itakayoitwa 2009, sasa nipo studio ya Sound Cfafters kwa ajili kurekodi hiyo singo,ambayo anaamini itawashtua wengi,kwamba aalahh hata Mkubwa Fella anaweza"alibainisha Mkubwa Fella

bongo mvua kiduuchu mtafutano


Bongo bwana mvua kiduuchu tu balaa kila mahali,Mvua ya kiasi imenyesha leo asubuhi jijini Dar,lakini adha ya msongamano wa magari na mifereji ya maji machafu kujaa imekuwa kero kubwa sana

nakuja na mambo mapya-Steve Nyerere


Steve Nyerere akiwa kwenye maandalizi makubwa ya kipindi chake ambacho kitahusisha mchakato mzima unaoizunguka jamii pamoja na wageni waalikwa ambao watakuwa wakichangia mada hizo kwa namna moja ama nyingine

Shoto ni Boss wa HATMAN PRODUCTIONS pamoja na mwanamuziki wa FM Academia Patchou Mwamba wakivutiwa na uandaaji wa kipindi cha Steve Nyerere talk show kitakachoanza kurushwa hewani mwezi ujao na televisheni ya TBC 1 jijini Dar

Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia kwa makini maandalizi makubwa ya kipindi cha Steve Nyerere talk show

Steve akimuigiza Rais Jakaya Kikwete wakati wa maandalizi ya kipindi chake

Msanii mchekeshaji na muigizaji wa sauti mbalimbali za watu maarufu ajulikanae kwa jina la Steve Nyerere akimuigiza Rais JK katika moja ya hotuba zake,hayo ni moja ya maandalizi makubwa na ya kufa mtu ya utengenezaji wa kipindi chake kitakachoitwa Steve Nyerere Talk Show kitakachokuwa kinarushwa na televisheni ya TBC hapa jijini Dar.Kipindi hicho kinachorekodiwa na kampuni ya HATMAN PRODUCTIONS kinatarajiwa kuanza kurushwa hewani mwezi ujao,haya wadau kaeni mkao wa kula mambo mapya yanakuja TBC.

NB: Ukimuhitaji Steve Nyerere katika shughuli zako mbalimbali wala usisite bofya namba hii 0715 782424 na utasikilizwa na kujibiwa haraka.

Askari wa JWTZ amuogesha dereva wa school bus



Hiyo picha nimetumiwa na mdau, naomba tuiwakilishe hivyo
hivyo japo haionekani vizuri:-

"Kaka naomba uiwakilishe hii picha ya askari wa JWTZ aliyemuogesha
dereva wa school bus pale kawe darajani kwa komba asubuhi ya leo baada
ya kumwagia maji viatu vyake ambavyo anadai alivipiga kiwi leo asubuhi.
Haya sio ya kusikia nimeyaona kwa macho na watu wadau wengine pia
alishuhudia. Hebu tuulize wana jamii; Mlinzi wa wananchi anapofanya kitu
hii wewe unapata picha gani?" Nawakilisha

NB:Wadau mimi kama kawaida yangu ya ujumbe,si mnajua mjumbe hauwawigi

kp na Busara zake !!

kikwangua anga cha kampuni ya nanihiii


Kikwangua anga kingine cha kampuni ya nanihii kikapandishwa taraatibu,ebwanaee bongo imecharuka kwa vikwangua anga si mchezo

Wednesday, January 28, 2009

bongo kutamu
maeneo ya mwanga


Blaza Kadidi, na mwenzio Kamanda Kombe

Nimekutumia hii picha niliyoipiga hivi punde, ili na wadau wengine wajionee Bongo isivyo tambarare.

Ni wiki mbili tu zimepita tangu ajali itokee huko Tanga kwa basi kuligonga nyuma lori lililokuwa limeharibika, pasi kuwa na vielelezo vyovyote kuwa limesimama kwa ubovu, na wala hapakuwa na reflectors nyuma ya lori hilo.

Hebu tazama hili gari ya takataka, hapa niliibamba ikikata kona, kutoka barabara ya M/nyamala kuingia Kawawa, indiketa zake hazifanyi kazi, taa za nyuma hata moja haiwaki, kibao cha namba hakipo, na huu wavu waliozuia nao uchafu unavujisha kidogo kidogo, thus uchafu ulikuw aunadondoka barabarani. Pia tairi zake kipara wakati limebeba mzigo mzito namna hii.

Swali; Hii inamaanisha traffic hawalioni? Au mnaliona na huwenda hawaruhusiwi kulikamata? au huwenda ndio linavyotakiwa kuwa kiuchafuuchafu?, au hili lori liue watanzania wangapi ndio mpate pa kuanzia kuchukua hatua ili tuione mnafachapa kazi?

Imagine gari kama hilo mdau linapata breakdown usiku, alafu unakuja nyuma yake itakuwaje? Natumai kama mhishimiwa fulani angekuwa na maono kuwa baada ya siku kadhaa gari yake ingejibamiza hapo nyuma ya hii lori, maamuzi yake ya leo yangekuwa tofauti.Au angekuwa na maono kuwa school bus alilopanda mtoto wake italivaa lori hili kwa nyuma, angechukua hatua flani leo. Kwakuwa haya yoote hatuwezi kuwajua ni bora kuchukua hatua leo.

Mdau MG
( Koplo wa polisi jamii)

Kesi ya twin tawa za BoT yaanza
twin tawa za bot
MAOFISA wa ngazi za juu katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba na Deogratius Kweka, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, wakikabiliwa na mashitaka matatu ya kutumia vibaya madaraka yao na kuisababishia Serikali hasara ya zaidi ya Sh bilioni 200.
Mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo Hadija Msongo jana, Wakili wa Serikali John Lwabuhanga alidai kuwa Liyumba ambaye ni Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa BoT na Kweka ambaye ni Meneja Miradi wa BoT, wanakabiliwa na mashtaka ya kutumia vibaya madaraka wakiwa watumishi wa umma.
Akiwasomea mashitaka, wakili huyo alidai katika mashitaka ya kwanza dhidi ya Liyumba kuwa, katika siku tofauti kati ya mwaka 2001 na 2006, akiwa mtumishi wa umma BoT, alitumia madaraka yake vibaya kwa kuchukua uamuzi wa kuandaa ujenzi wa jengo la BoT bila kufanya makubaliano na Bodi ya Uongozi wa BoT.

Soma stori nzima kwa

KUBOFYA HAPA

New Tanzania Music

ISHIKE RADIO PART 11 street album(AFRICAN BANTU EDITION), available now for FREE download! Includes TZ artists like Matonya, TID, Chidi Benz, Q-Jay, Mwana FA, Hussein Machozi, Ngwea, Mr Blue and many moreThe street album is hosted by Bamboo the African BantuThe album features new and exclusive music from Bamboo plus tons of world premiers from various artists. One thing I will say is that I break records on an international platform so like Sparks says "Get Familiar". With this ISHIKE RADIO SERIES I showcased various African artists plus other artists based across the world to create that international vybe. ISHIKE!!!!!!!
Tracklisting
1. Ishike Radio Part 11 Intro (Produced By Dj Dona)
2. Bamboo Intro
3. Bamboo Feat K-Nel - Swagger Like Us (Remix)
4. Bamboo - Tabia Mbaya
5. Chidi Benz - Dar Stand Up (Ngoma Itambae)
6. Ron Browz- Jumpin Out Of Window
7. Hussein Machozi Feat DNA - Full Shangwe
8. Longombas - Queen
9. Amani - Tonight
10. 9ice - Gongo Aso
11. Prezzo Feat Tah Blaze- Cheki Navyo Roll
12. Nipsey Hustle Feat Game - They Roll
13. Bamboo -Tubambiane
14. Bamboo/K South Interlude
15. Doobiez - One 4 Hip Hop
16. Willy Northpole- 300
17. K-Nel - Tingiza (Quamtum Riddim)
18. Ngwea Feat. Juma Nature - Mida Mibovu
19. Bamboo Feat Archapello and K-Nel - Bambika (ISHIKE RADIO EXCLUSIVE)
20. Dj Felli Fel Feat. T-Pain, Sean Paul, Flo-Rida & Pitbull - Feel It
21. Indiginas - Parararera
22. Matonya Feat. T.I.D - Sina La Kufanya
23. Bamboo Interview
24. Bamboo- Jaza Ma Rhymes
25. P-Unit - Juu Tu Sana
26. Mejja- Pesa Kwa Bank
27. K-Naan - Somalia
28. French Montana, Dame Grease & Max B-Goon Musik
29. Mwana Fa Feat. Mr Lennny -Sema
30. Bamboo - Mama Africa
31. Kardinall Offishall Feat Dr Dre and Clipse - Set it Off
32. Hussein Machozi - Kafia Ghetto
33. Ken Razy, Kaya, DNA - Mziki
34. Mr Blue Feat Steve - Tabasamu
35. Q-Jay - Mwenyewe
36. Howee - Sorry Mama
37. Bamboo Outro -- ISHIKE!!!!!DJ DonaDj/Producer

“Malkia
Bridal Collection 2009

Your Once in a LIFETIME INDULGENCEBy Mustafa Hassanali. Mustafa Hassanali shall launch his DEBUT BRIDAL COUTURE Collection for the year 2009, on SATURDAY February 7 at the The Little Theatre Club, Next To ST. PETERS CHURCH on Haille Sellasie Road “Malkia” is proudly sponsored by ZAIN, STELLA ARTOIS and MOTOMEDIA

JK amtembelea mpiganaji Athumani Hamisi sauzi
JK akimjulia hali mpiga picha wa magazeti ya Serikali ya Daily News na HabariLeo, Mpiganaji Athuman Hamisi Msengi, wakati alipomtembelea kwenye Hospitali ya Milpark (pichani chini) ya mjini Johannesburg, Afrika Kusini jana baada ya kikao cha wakuu wa nchi za SADC. Mpiganaji Hamisi amelazwa baada ya kupata ajali ya gari huko Kibiti, Mkoa wa Pwani, takriban miezi mitatu ilopita na kupata majeraha kwenye shingo na uti wa mgongo. Hali yake inaendelea vizuri japo maungo bado hayafanyi kazi sawasawa. Picha na mdau Juma Kengele wa Ikulu



Survival for the fittest....!!!!

Ndo maisha yalivyo....hususan kwa wanyama wasio na utashi......... mbabe ndo anaendelea kula hewa ya hii dunia......!!! sio lazima iwe porini tu.... ata uraiani....!!!

Tuesday, January 27, 2009

Mnaokuja Dom muwe macho....!!!

Eneo la mlima uliyopo dodoma makulu ambapo alimanusura matapeli watatu wawili kutoka dsm wakiwa na mwenyeji wao wamlize babu wa watu kutoka rombo kiasi cha sh40m...fedha ambayo babu huyo aliipata baada ya kuuza nyumba yake iliyopo dsm.... hata hivyo polisi mkoani dom walistukia game na kumwokoa babu huyo asitapeliwe......
Eneo hili ndilo babu huyo toka rombo alipoambiwa kuwa atazungumza na babu anayeweza fanya mazingara chapaa hizo Sh40m zikawa Sh600m.....
Hapa kuna mishumaa pamoja na udi ambayo huwashwa na kumpumbaza mtapeliwa kuwa ataongea na maruhani.... ila kwa mbele kama anapoelekea kamanda mmoja pichani kuna tundu la kutokea upande wa pili.... ila kwa juu yake kuna madondora kichizi.....!!!

Beware!

WIZI ULIONIKUTA

Nimeonelea ni vema niwajulishe mbinu hii ya wizi ili isiwa fike nanyi .

Kuna kijana ambaye anadai ametoka Morogoro na ametumwa na mzee wake kununua gari kumbe ni taperi na mwizi .
Kwa kadiri ya wiki mbili kijana alikuwa akifuatilia Gari ambayo nilikuwa naiuza na nikaitangaza katika Dar – Advert . Alisema yakuwa yeye yuko Morogoro na anahitaji kuiona gari ; mnamo tarehe 25 / 12 / 2008 asubuhi , tulipokea simu yakuwa tukutane na kijana ambaye ameondoka morogoro tumuuzie hilo gari . ( Na mpigaji akiwa ni mzee wake kutoka Morogoro; baada ya muda kijana aliomba udhuru ya kuwa tarehe 25 ni Krismasi baba yake angependa aje kuangalia hilo gari ila yeye hataweza atafika tarehe 26 / 12 / 2008 .

Saa moja asubuhi tarehe 26/12/08 alipiga simu na tukaelewana tukutane naye B.P petrol station Mbezi Beach ..tulipokutana alicheki gari kama mnunuzi yeyote kutoka bodi mpaka engine.akaomba afanye road test –he is a good driver
Alionyesha kuridhika na gari na kuonyesha nia ya kulipia fedha ambayo alikiri iko kwa jamaa ya baba yake aliyepo jmall ambaye ni agent wa oilcom.; alipotoka j mall alidai amepewa fedha ambayo ni dollar hivyo ilibidi tuende mlimani city kubadili fedha na kudeposit kwenye account kwani anasisitiza hapendi kulipana fedha mkononi angependa tulipane bank.

Tulipokuwa ndani ya bureau de change alikuwa akiwasiliana na jamaa zake na simu yake ilizima kwa kukosa chaji hivyo aliomba simu yangu kwa mawasiliano pia alielezea juu ya hali yake kuwa amekunywa dawa amoxyline na tumbo linamsumbua kwani hajapata kifungua kinywa hivyo angependa kwenda kuchukua maziwa hivyo alitoka nje huku akiwasiliana kwa kutumia simu yangu.
Kwa vile nilishakaa naye kwa muda upatao masaa matatu na juu ya yote alikuwa ameacha bahasha yake ya dollars tulipokuwa tumekaa sikupata wasiwasi naye kabisa.
Alipotoka ndani tu katika dakika tano nilishuku hivyo nikafungua bahasha yake kuchungulia mzigo wa dolla nikakuta ni magazeti yaliyofungwa vizuri haikuchukua dakika kumi watu ambao contact zao zilikuwa ndani ya simu yangu walipokea message iliyosomeka ifuatavyo
“ naomba unitumie vocha ya 5000/= nitakurudishia niko sehemu hapana duka na nahitaji sasa hivi”
Watu wengi waliibiwa kupitia kutumtumia dolla.
Ninawataarifu jambo hili kwani nimegundua limemtokea na mwenzangu ofisini siku ya jumapili 21/12/08 na mimi nilituma dolla nikifikiri namsaidia kumbe naibiwa. Kwa huyu mwenzangu mbinu iliyotumika ni sawa kabisa na mbinu iliyotumika kwangu.nina wasiwasi wengi watalizwa na kijana huyu.
Kijana ni smart, knowledgeable, polite looking, courageous na kimwili ni mdogo mdogo and very friendly during the discussions si rahisi kumshuku

Kinachonisikitisha kijana yuko bright laiti angalitumia hizi sifa zake kufanya kazi rasmi naamini angekuwa mbali sana
Haya …bomu hilo kaeni macho!!!!!!peleka ujumbe huu kwa watu wowote utakaoweza ili kupunguza tatizo.

Kumbe hii ndio bahi….!!

Mbuzi aliyekuwa akila ride juu ya kichwa cha scania akiangalia mandhari ya bahi wakati lori hilo lililokuwa safarini liliposimama kwa muda maeneo hayo …..

MADEREVA BWANA.... NOMA KICHIZI....!!!!

Haya sasa.... huyu naye tena anamdraiv mheshimiwa... ila angalia alipoegesha gari.....!!!!
Huyu naye baada ya kumwaga mchanga.... tipa limekataa kurejea sehemu yake.... akaamua kutambaa hivyo hivyo.... huku deiwaka wake akiwa nyuma kimashakamashaka....!!!
Mwingine kaamua tu kudharau ishara ya barabarani (kushoto) inayomwonyesha kuwa hiyo ni njia moja tu.... hairuhusu gari kuenda upande anaoelekea...........!!!!

MADEREVA BWANA.... NOMA KICHIZI....!!!!

Haya sasa.... huyu naye tena anamdraiv mheshimiwa... ila angalia alipoegesha gari.....!!!!
Huyu naye baada ya kumwaga mchanga.... tipa limekataa kurejea sehemu yake.... akaamua kutambaa hivyo hivyo.... huku deiwaka wake akiwa nyuma kimashakamashaka....!!!
Mwingine kaamua tu kudharau ishara ya barabarani (kushoto) inayomwonyesha kuwa hiyo ni njia moja tu.... hairuhusu gari kuenda upande anaoelelea...........!!!!

Vichwa TRL kweli vimechoka....!!!! Kumbe ndo maana enz za mwl waliitaga gari moshi...!!!

Injini ya treni ikitoka stesheni ya dom njiani kuelekea bara..... kilichonivutia ni hali ya utoaji moshi mwingi mno..... hii ni moja kati ya uchafuzi wa hali ya hewa........!!!

BORA ATCL IONDOKANA NA HAYA....!!!

Bila huruma ya sirikali.... Any Time Canceled Limited ingewafika haya.....!!!

Watoto wa mitaani ni tatizo kichizi dom

Kijana aishie katika mazingira magumu akiwa amelala katika bustani ya Nyerere mjini Dodoma. Idadi ya watoto kama hawa inazidi kuongezeka mkoani Dodoma ambapo takwimu zinaonyesha kuwa kuna zaidi ya watoto elfu 14 wanaoishi katika mazingira magumu mkoani humu, ambapo asilimia 62 ya idadi hiyo bado wapo mitaani.

Wednesday, January 21, 2009



RTO-IRINGA ISIWE NGUVU YA SODA

Mhariri,

NAFURAHI kusema kwamba nimefurahishwa na RTO-Iringa bwana Mnubi ambaye kama sijakosea ni senior superitendant kicheo.Bwana huyu juzi tarehe 19/01/ 09 alitusimamisha pale Iringa{check point} na kuanza kukagua magari yote yanayosafiri mikoa ya jirani kupitia mkoa wake.Akishirikiana na vijana wake pamoja na mkaguzi wa magari wa polisi wa mkoa,walikagua kama kila gari lina dereva wa ziada pia kama linakidhi mahitaji ya kusafiri safari ndefu,kwa magari ambayo hayakukidhi sheria hizo yalitozwa faini ya shilingi laki moja kama faini au kumwacha kondakta apelekwe kortini na wengine kuruhusiwa kuendelea na safari.

Kwa kitendo hicho kililaaniwa na abiria wengi wakiwemo wa basi nililokuamo HOOD la Tunduma wakidai kwamba wanacheleweshwa bila kujua kwamba RTO na timu yake wako kazini pia wako pale pia kulinda haki ya abiria na kupunguza ajali barabarani cha kushangaza ni kwamba abiria wa basi langu na mabasi mengine walianza kumzomea na kumtukana RTO wakisahau haki yao ya kufika salama,ni muhimu madereva kupokezana hasa kwa safari ndefu kwani siyo nzuri kiafya pia umakini barabarani unapungua kwa sababu akiwa mmoja anachoka.

Binafsi naunga mkono kazi ya RTO-Iringa ila TU ISIWE NGUVU YA SODA.Kwa kufanya hivyo itasaidia kupunguza ajali barabarani natoa rai abiria tusiwe tunatetea upumbavu unaofanywa na madereva kama waliofanya basi nililokuamo na mengine.Pia vita ya kupunguza ajali si ya askari polisi tu bali na abiria pia kwani wao ndiyo walengwa wakuu.

Hii iwe changamoto kwa ma RTO wengine kwani kutokua kwao makini kunawapa kiburi madereva na madereva wanamwona RTO –Iringa mnoko wakati yuko kazini.Chakushangaza tulitoka Dar,Pwani na Morogoro lakini hatukukaguliwa hii inanipa picha ya UZEMBE wa ma RTO wa mikoa hiyo.Hivyo pongezi kwa RTO-Iringa na timu yake, pia Iringa iwe ni mfano ,

kwani mabasi hubeba roho za watu na si mawe.

Kasuga (mzee wa muliko),


Tuesday, January 20, 2009

Tunakukumbuka Bibi Yetu
Delphina Kasuga .

Bibi yetu Delphina Kasuga kesho tarehe 21/01/2009 tutakuwa tunafikisha mwaka wa tatu tangu ututoke katika ulimwengu huu pale hospitali ya Mama Ngoma ilikuwa ghafla sana ingawa tulikupenda sana ila Mungu alikupenda zaidi.
Wajukuu zako tunakukumbuka sana Ronald Kasuga, Fina Kasuga ,Joshua Kasuga, Rose Lema, Ferald Akyoo, Magdalena Akyoo, Safari Kawa, Agustino Kasuga, Babu na wengineo wengi neo wengi ulioshirikia na nao kwa ukaribu .
Tutakukumbuka Daima .
Raha ya milele umpe Ee Bwana na mwanga wa milele Umwangazie Astarehe kwa Amani Amina .

Monday, January 19, 2009


Baada ya ziara za mikoani na kumwaga sumu katika Operesheni Sangara sasa Viongozi wa Chadema wameingia jijini Dar es Salaam kuendeleza operesheni hiyo.
tarehe 12 ndio walitanagaza rasmi kuvunja ndoa na vyama vingine vya upinzani!!
Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe amesema wamegundua kuwa kuna vyama vingine ambavyo ni mamluki katika upinzani na hivyo Chadema kitapambana chenyewe kuwakomboa waTz ila jamani kuna ya ccm inaitwa nyavu kama sikosei kwa hiyo hapo ni raha tupu hiyo wameizindua kutoka Arusha .
Mlimani Mambo
Magumu....
JESHI la polisi limelazimika kuvunja maandamano ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,yaliyokuwa yameandaliwa na serikali ya wanafunzi iliyoripotiwa kutotambuliwa chuoni hapo (DARUSO).Maandamano hayo yaliandaliwa kwa lengo la kupinga utaratibu wa udahili unaoendelea kwa kuwarudisha wanafunzi ambao wamekamilisha malipo yao yote.Mwananchi ilishuhudia wanafunzi wakiwa nje ya chuo wakijiandaa kuandamana huku wakiwa wameshika mabango yanayochochea maandamano, huku wengine wakiwa wanaendelea na udahili kama kawaida.
"Tumeamua kuandamana leo uongozi uone wenyewe kwamba unachokifanya sio halali kwani kumrudisha kuendelea na masomo mwanafunzi mwenye uwezo na kumuacha asiye na uwezo ni sawa na ukandamizaji,"walisikika wanafunzi hao wakiwa wameshikilia mabango tayari kwa maandaamano."Habari ya Hussein Issa na Picha ya Emmanuel Herman.
Mramba ruksa kuhudhuria vikao vya Bunge
Waziri wa zamani wa Fedha, Basil Mramba, ameruhusiwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, kuhudhuria Mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu. Hata hivyo, mahakama hiyo imesema inaweza kumwita wakati wowote itakapomhitaji kwa sababu mbalimbali zinazoweza kujitokeza. Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Hezron Mwankenja, alisema jana kuwa ametoa uamuzi huo baada ya kusoma vifungu mbalimbali vya Katiba na kuona hakuna sababu ya kumzuia. ``Lakini tufahamu kuwa ruhusa hii, haizuii mahakama kumwita wakati wowote itakapomhitaji hata kabla ya tarehe ya kusikiliza kesi yake ambayo ni Februari 2 mwaka huu,`` alisema. Alisema Ibara ya 17 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inatoa fursa ya uhuru wa mwananchi kutoka sehemu moja ya nchi kwenda nyingine. Vilevile, Mwankenja alisema Ibara ya 13 (6) (b) (Presumption of Innocense), inasema mahakama pekee ndiyo yenye uwezo wa kumtia hatiani mshtakiwa hivyo kumyima ruhusa ya kusafiri ni sawa na kumhukumu kabla hajatiwa hatiani na mahakama. ``Justice must be done and seen to be done`` alisema Mwankenja akimaanisha kuwa haki lazima itendeke na ionekane dhahiri kuwa imetendeka. Hata hivyo, Mwankenja alisema Sheria za Bunge hazijaweka wazi kuhusu utaratibu mbunge anapopatwa na matatizo kama ya Mramba. Hakimu alisema Dodoma ni karibu hivyo ni rahisi kwa mshtakiwa huyo kusafiri mara moja na kufika Dar es Salaam endapo atahitajika, hivyo hakuna sababu yoyote ya kumzuia kusafiri. Alisema wadhamini wake lazima waarifiwe kuhusu ruhusa hiyo ya kusafiri ili wasiwe na hofu. Kesi ya Mramba na mwenzake Daniel Yona itatajwa tena tarehe 2 mwezi ujao. Mramba aliwasilisha ombi hilo kupitia wakili wake Herbert Nyange Januari 2 mwaka huu akitaka ruhusu ya kwenda jimboni kwake. Barua ya ombi hilo ilielekezwa Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo ikitaka ruhusa ya kuwa nje ya Jiji la Dar es Salaaam kuanzia Januari 3 mwaka huu hadi mwezi ujao. Mramba na Yona wanakabiliwa na makosa ya kutumia madaraka yao vibaya kwa kuipatia mkataba wa kukagua uzalishaji wa dhahabu kampuni ya Alex Stewart (ASSAYERS) ya Uingereza na kampuni yake tanzu ya Alex Stewart (ASSAYERS) Government Business Corporation, kinyume cha Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2002 na ile ya Madini ya mwaka 2002. Katika shitaka la pili, Mramba na Yona wanadaiwa kuwa Mei 28, mwaka 2005 wakiwa watumishi wa umma jijini Dar es Salaam, wakiitumikia serikali katika nafasi za uwaziri wa Fedha na Nishati na Madini, kwa pamoja walitumia vibaya madaraka yao kwa kusaini mikataba ya kuiongezea kampuni hiyo muda wa miaka miwili wa kuendelea kukagua madini ya dhahabu kuanzia Juni 2005 hadi Juni 2007 kinyume cha Sheria ya Manunuzi ya Umma.
SOURCE: Nipashe
Kipanya na busara zake ..

Saturday, January 3, 2009


UTAMU WATOWEKA MBEYA
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imetupilia mbali rufaa ya mgombea wa Chadema kupinga kuenguliwa kwenye kinyang'anyiro cha ubunge wa Mbeya Vijijini. Mgombea wa Chadema, Sambwee Shitambala (pichani aliyenyanyua vidole vya ushindi)alienguliwa na Tume ya Uchaguzi ya Mbeya Vijijini baada ya vyama vya CCM na CUF kuwasilisha pingamizi, vikidai kuwa alikiuka Sheria ya Uchaguzi kwa kuapa kwa wakili badala ya kwa hakimu.Mgombea huyo ambaye ni mwanasheria, hakukubaliana na uamuzi huo na kukata rufaa Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Lakini leo, mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji Lewis Makame aliwaambia waandishi wa habari kwenye hoteli ya Mount Livingstone kuwa baada ya kutafakari mambo makuu manne, tume yake imetupilia mbali rufaa hiyo.

mgonja aunganishwa na akina mramba na yona



Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam, jana imemuunganisha aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Grey Mgonja, katika kesi ya watuhumiwa wengine wa ufisadi, Basil Pesambili Mramba na Daniel Yona.

Wote hawa wanakabiliwa na tuhuma za kutumia vibaya madaraka yao na kulisababishia taifa hasara ya takribani bilioni 11.Hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Hezron Mwankenja alifikia hatua hiyo kufuatia ombi la upande wa utetezi katika kesi ya Mgonja unaoongozwa na Profesa Leonard Shaidi, kuiomba mahakama hiyo kumuunganisha mteja wake na akina Mramba na Yona kwa kile alichodaiwa kuwa kesi hizo zinafanana.

Pichani aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba (kulia) akiteta jambo na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Daniel Yona (katikati) wakati walipokuwa mahakamani, mapema mchana hii leo Kushoto ni Grey Mgonja.

mmh mambo ya funga mwaka haya.!