Wednesday, January 28, 2009

Kesi ya twin tawa za BoT yaanza
twin tawa za bot
MAOFISA wa ngazi za juu katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba na Deogratius Kweka, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, wakikabiliwa na mashitaka matatu ya kutumia vibaya madaraka yao na kuisababishia Serikali hasara ya zaidi ya Sh bilioni 200.
Mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo Hadija Msongo jana, Wakili wa Serikali John Lwabuhanga alidai kuwa Liyumba ambaye ni Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa BoT na Kweka ambaye ni Meneja Miradi wa BoT, wanakabiliwa na mashtaka ya kutumia vibaya madaraka wakiwa watumishi wa umma.
Akiwasomea mashitaka, wakili huyo alidai katika mashitaka ya kwanza dhidi ya Liyumba kuwa, katika siku tofauti kati ya mwaka 2001 na 2006, akiwa mtumishi wa umma BoT, alitumia madaraka yake vibaya kwa kuchukua uamuzi wa kuandaa ujenzi wa jengo la BoT bila kufanya makubaliano na Bodi ya Uongozi wa BoT.

Soma stori nzima kwa

KUBOFYA HAPA

No comments: