Thursday, January 29, 2009

mkubwa fella aja na singo yake kuleta heshima


Anaitwa Said Fella lakini unaweza ukaanza kumuita kwa jila la Mkubwa Fella nae bila hiyana huitika kwa bashasha kabisa.Kwa wale wasiomfahamu vyema ni yule meneja wa kundi la Wanaume TMK Familly lenye makao yake makuu kule kule Temeke jijini Dar.

Mkubwa Fella amenitonya hivi punde kwa njia ya simu kwamba ameingia studio ya Sound Crafterz kwa ajili ya kurekodi singo yake ya kwanza itakayoitwa 2009.Amesema kuwa anataka kuwaonesha baadhi wasanii ambao wamekuwa wakimfuata wakati wa shida na kusaidiwa, wakishiba wanakuja na maneno ya kashfa na kiburi kama baadhi ya wasanii wengine ambao wamekuwa wakimtuhumu kwa maneno ya hapa na pale.

"Nataka kuwaonesha baadhi wasanii kuwa hata mimi na naweza,ili kuthibitisha hilo wakae mkao wa kula nakuja na singo yangu ya kwanza itakayoitwa 2009, sasa nipo studio ya Sound Cfafters kwa ajili kurekodi hiyo singo,ambayo anaamini itawashtua wengi,kwamba aalahh hata Mkubwa Fella anaweza"alibainisha Mkubwa Fella

No comments: