Sunday, August 30, 2009

England premier league
England - Premier League
06:12August 29

FTChelsea3 - 0Burnley

FTBlackburn R.0 - 0West Ham U.

FTBolton W.2 - 3Liverpool

FTStoke C.1 - 0Sunderland

FTTottenham H.2 - 1Birmingham C.

FTWolverhampton W.1 - 1Hull C.

FTManchester U.2 - 1Arsenal
RAMADHAN KAREEM
Leo ni Ramadhani 9

Ninawatakia wadau WaIslamu wote Mfungo Mwema wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

By
Kadidi2
MAMBO YA HASHEEM BONGO





Mjomba Hasheem anaetuwakilisha huko ughaibuni katika ligi bora ya kikapu duniani akiwa kwa mapumziko akijifua kidogo katika uwanja alioanzi harakati za kuelekea kwenye mafanikio aliyokuwa nayo kwa sasa .
Kaka kila la kheri na pia tuanshukuru kwa kuwa na balozi wa kitanzania katika ligi hiyo na pia kwa kumbukumbu zangu kama nzuri na pia ni mtanzania wa kwanza katika ligi hiyo. Nani atamfuata hatujui tusubiri tuone !!!!!!!!!!!
mdau kiluke angára katika karate japan
Mdau Kiluke akiwa kwenye mashindanoya kimataifa ya karate.
yaliyofanyika Hachioji Tokyo ambapo alishinda kwa pointi nyingi
Mdau Kiluke akiwa na washindi wenzie
Mdau Kiluke akipokea nondozzz ya ushindi wake. Wabongo tumo nasi...


UZINDUZI WA FILAMU:CONFUSION IN ROCK CITY
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe. Abbas Kandoro akizindua filamu ya ‘Confusion in Rock City’ akiwa na Ruge Mutahaba, mtunzi wa sinema hiyo katika hoteli ya Nyumbani ndani ya NSSF Plaza Mwanza
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Afande Jamal Rwambo, Kemmy Mutahaba, mratibu wa filamu hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Abbas Kandoro na Ruge Mutahaba wakipongezana baada ya sinema hiyo kuzinduliwa rasmi.

Waziri wa Nishati na Madini Mh. William Ngeleja (pili shoto) akiwa na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa ATCL William Haji (shoto) na washiriki wa filamu ya Confusion in Rock City. ATCL walikuwa wadhamini wakuu kwenye utayarishaji na uzinduzi wa sinema hiyo ambayo iko madukani nchi nzima.



Askari wa KAR kuhakikiwa
askari wa KAR katika tizi la gwaride enzi hizo
Serikali imewataka askari wa King's African Rifles (KAR) waliopigana vita kuu ya pili ya Dunia kuripoti katika ofisi za Mkuu wa mkoa au wilaya zao wakiwa na vitambulisho au vielelezo husika kwa ajili ya uthibitisho wa kutambuliwa .

Katika taarifa iliyotolewa hivi karibuni na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa yamehorodhesha majina ya askari wote waliopigana vita hivyo vya mwaka 1939 hadi 1945.

Taarifa hiyo inasema kuwa orodha ya majina ya askari hao inapatikana katika ofisi zote za mikoa na wilaya za Tanzania bara na Visiwani.

Mikoa hiyo ni Tanga, Arusha,Mjini Magharibi , Unguja na ofisi za wilaya ya Tunduru, Songea, Nchingwea, Bunda, Serengeti, Bahi, Geita, Temeke, Kisarawe, Ilala, Maswa, Babati, Morogoro, Mvomelo, Iringa, Kyela, Singida na Dodoma mjini.

Wilaya nyingine ni Kishapu, Masasi, Shinyanga, Kilosa, Karangwe, Kondoa, Tabora, Nzega, Mpanda, Kongwa, Biharamulo, Igunga, Misenyi, Muleba, Handeni, Namtumbo, mkoa wa mjini Magharibi na unguja, Wilaya ya Magharibi na Kusini Unguja.

Pia katika orodha hiyo ya majina kuna majina ya askari wa KAR ambao hawajulikani maeneo waliyotoka.

Zoezi la uhakiki wa askari hao limeanza kufanyika tangu tarehe 15/8/2009 na litamalizika tarehe 30/10/2009.

BODI YA UKAGUZI WA FILAMU YAZINDULIWA, UONESHAJI HOLELA WA SINEMA SASA MARUFUKU
Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo George Mkuchika akizungumza na wafanyakazi wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo wakati wa uzinduzi wa Bodi ya Ukaguzi wa Filamu jana jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Utamaduni Pof.Hermas Mwansoko,akifuatiwa na Beneventus Lopa Afisa Mipango na Utawala wa Wizara hiyo na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Bw. Clement Mshana
Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo George Mkuchika akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Bodi ya Ukaguzi wa Filamu mara baada ya uzinduzi.Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Bodi hiyo Bi. Rose Sayore. Picha na habari na Aron Msigwa- MAELEZO.

Serikali imepiga marufuku maonyesho yote ya filamu kwenye hadhara ya watu, majumba yasiyo rasmi,vibanda ,kumbi ndogondogo, hoteli na maeneo ya baa bila kufuata masharti ya jumba la sinema na kwa mujibu wa sheria na 4 ya mwaka 1974 inayotumika nchini.

Agizo hilo limetolewa leo jijini Dar es salaam na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo George Mkuchika wakati wa Uzinduzi wa Bodi ya Ukaguzi wa Filamu nchini ambayo itakuwa na jukumu la kukagua na kusimamia maonyesho na shughuli za filamu nchini.
Amesema sehemu nyingi zinazotumiwa kuonyesha filamu hazina leseni halali za kuonyeshea filamu na kuongeza kuwa sio salama kwa mali na afya za watu.
“Nachukua fursa hii kutoa onyo kwa mtu yeyote atakayeonyesha filamu kwenye hadhara ya watu katika majumba yasiyo rasmi ,vibanda,kumbi ndogondogo,hotelini, baa na katika vyombo vya usafiri waache mara moja” amesisitiza.

Amefafanua kuwa sehemu nyingi zinazotumika kuonyeshea filamu sasa hazikidhi matakwa ya ujenzi wa kumbi za kuonyeshea filamu na ni kinyume cha sheria kwani nyingi zimekuwa chanzo cha maficho ya wahalifu, majambazi, biashara ya dawa za kulevya na kuchochea vitendo vya ngono kwa vijana.
Amesema athari nyingi tayari zimeshajitokeza katika jamii yetu na kuongeza kuwa filamu nyingi zimechangia kubomoa na kudunisha Utamaduni wa taifa letu na hata kuchangia kwa kiasi kikubwa kubomoa misingi ya amani , Upendo , Uadilifu,heshima, uaminifu na utu ambao ni utambulisho wa mtanzania jinsi ulivyokuwa umejijenga na kuenea katika jamii yetu.

Waziri Mkuchika amewataka wanaojishughulisha na shughuli za kuonyesha filamu kwa kuzingatia sheria na kufuata kanuni za nchi licha ya kuwa ya fani ya filamu kukuza ni biashara na inakuza uchumi na pia kuleta maendeleo na kuwataka kuepuka kuonyesha filamu zinachochea vitendo viovu na mmomonyoko wa maadili ndani ya jamii kutokana na filamu nyingi kutokaguliwa na kupangwa katika madaraja kulingana na matakwa ya watanzania.

Aidha amesema serikali iko makini kuhimiza na kusisitiza matumizi ya sanaa katika masuala mbalimbali ya maendeleo na kuvitambua , kuvikuza na kuviendeleza vipaji vya wasanii katika kukuza taaluma na fani ya filamu nchini.
Awali akizungumza kuhusu majukumu ya Bodi hiyo amesema kuwa Bodi itakuwa na jukumu la kuweka misingi ya kuimarisha utaratibu wa usimamizi wa utengenezaji wa filamu na pia kutoa vibali vya kutengeneza filamu hapa nchini.

Mbali na jukumu hilo Bodi ya Ukaguzi wa Filamu itakuwa na jukumu la kuratibu, kusimamia na kushauri namna ya kukuza Tasnia ya Filamu kwa kuzingatia sera ,sheria na kanuni zikiwemo taratibu na miongozo mbalimbali ya nchi hasa sera ya Utamaduni na Sheria ya Filamu na Michezo ya kuigiza.

Naye Mwenyekiti wa Bodi hiyo Bi. Rose Sayore ameihakikishia serikali kuwa Bodi yake itafanya kazi kwa mujibu wa sheria na kuhakikisha kuwa kanuni, sheria , maadili na taratibu za uonyeshaji na utengenezaji wa filamu zinazingatiwa kwa maslahi ya watanzania na vizazi vijavyo.

Dk. buriani azuru bandari ya uvinja nchini kongo
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Dk. Batilda Buriani wakitembelea Bandari ya Uvinja katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Mheshimiwa Deogratias Ndunimana Waziri wa maji na Mipangomiji Burundi wakati wa Mkutano wa Tatu wa Nchi Zinazounda Mamlaka ya Usimamizi wa Endelevu na Ziwa Tanganyika HIvi Karibuni
Haya haya Kuelekea 2010

Wadau watumiaji wa barabara yetu ya mabibo hadi kigogo muda mfupi kabla ya uchaguzi wanaweza wakaanza kupata matunda ya barabara mzuri ila tuombe Mola mambo yaende kasi kama sasa yanavyokwenda maana simnajua tena barabara ikiwa ya lami mambo huwa bam bam hatuvunji magari na tunatumia muda mfupi barabarani na pia itapunguza kidogo foleni zetu za kati kati ya jiji.
Hongereni mamlaka husika kwa kusikia kilio chetu wakazi wa mabibo nyuma ya soko.
Ni mimi mdau ,Mpenda maendeleo.

Thursday, August 27, 2009

nishati bwelele makete

HAYA NI MAPOROMOKO YA MTO LUVANYINA AMABAO HAUKAUKI MWAKA MZIMA. UPO KATA YA KIPAGALO TARAFA YA BULONGWA WILAYA YA MAKETE. YANAZALISHAUMEME MWINGI TU NA HOSPITALI YA BULONGWA IMEKUWA IKITUMIA UMEME HUU YENYEWE NA WANANCHI WA TARAFA ILE. Je Tanesco hawawezi kuona hili??
Mdau Josephat wa Makete
maji yakienda kwa kasi kwenye mtambo wa kuzalishia umeme
kwa msiofika Makete haya ndio baadhi ya mandhari yake



matusi ya cafu wa brazil

video

bofya mshale uone video hii

kp na busara zake


kp na busara zake


vijimambo vya nathan mpangala
hasheem thabeet kwenye vekesheni bongo
akiwa vekesheni hapa bongo nyota wa mpira wa kikapu hasheem thabeet ana usafiri na ulinzi maalumu. leo asubuhi alikuwa katika mahojiano katika kipindi cha michezo cha kila jumatano cha radio one kinachoandaliwa na mtangazaji jezi namba tisa mgongoni maulidi baraka wa kitenge. pamoja na mambo mengine hasheem ametoa wito wa wachezaji wa kila mchezo wawe na chama chao cha kutetea maslahi yao

nizar khalfani akichakarika canada
nizar na wenzie wakishangiliwa baada ya kumtungua mtu
nizar akinyanyasa
akitawala kiuongoni
keshalizwa mtu
picha hizi za Nizar Khalfan akitutoa kimasomaso huko ughaibuni katika mechi ya Vancouver White Caps na Miami Picasa ambapo timu ya kina Nizar ilishinda na yeye alichangia sana ushindi huo. Naamini kabisa kuna baadhi ya wadau wa hili libeneke wangependa kabisa kuziona ili wapate kufarijika!!
Mdau DM

msaada tutani

naomba wajuzi wa lugha yetu mwanana ya kimatumbi wanisaidie maana hili linalinitatizaga sana kila nikipita ilala na kuona jengo hili ambalo limeandikwa "Chama Cha Walimu". Swali langu ni je lugha sahihi hapo ni ipi "Walimu" ama "Waalimu??"
Mdau Martin

sherehe za jeshi la wananchi kutimiza miaka 45
Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange akitoa maelezo kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya mambo ya nje Ulinzi na Usalama Wilison Masilingi mara baada ya ufunguzi wa maadhimisho ya JWTZ kutimiza miaka 45. Mh. Masilingi alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa Maadhimisho hayo yanayoendelea katika kikosi cha 603 cha jeshi eneo la Airwing ,Ukonga jijini Dar es salaam.Wa kwanza Kulia ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein mwinyi ambaye aliambatana na Naibu wake Dkt. Emannuel Nchimbi (wa kwanza kushoto).
Baadhi ya wananchi wakijitokeza kuangalia maonesho ya wiki ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ) kutimiza miaka 45 wakipata maelezo kuhusu silaha za kivita kutoka kwa wataalam wa Jeshi hilo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya mambo ya nje, Ulinzi na Usalama Mh. Wilson Masilingi akipata ufafanuzi kutoka kwa Luten Kanali Anselum Bahati kuhusu bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na JWTZ kikosi cha Nyumbu wakati wa maonyesho ya miaka 45 ya JWTZ.Kushoto ni Mkuu wa Majeshi Generali Davis Mwamunyange


Wananchi wakijitokeza katika mabanda ya huduma za tiba kwenye maonyesho ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania kutimiza miaka 45
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye maonyesho ya JWTZ kutimiza miaka 45 wakipata huduma za tiba na ushauri leo katika mabanda ya Maonyesho katika viwanja vya kikosi cha 603 cha Jeshi la wananchi Air wing,Ukonga jijini Dar es salaam.




Mkuu wa Majeshi Generali Davis Mwamunyange na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya mambo ya nje Ulinzi na Usalama Wilison Masilingi (kushoto kwa afande Mwamunyange) wakipata maelezo mara baada ya ufunguzi wa maonesho na maadhimisho ya JWTZ kutimiza miaka 45. Mh. Masilingi alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa Maadhimisho hayo yanayoendelea katika kikosi cha 603 cha jeshi eneo la Airwing ,Ukonga jijini Dar
Askari wa kikosi cha anga katika maonesho hayo
Wanafunzi wakiangalia baadhi ya silaha katika maonesho hayo
Askari wenye silaha za kutungua ndege katika maonesho
Wananchi wakiangalia vifaa vya kijeshi kwenye maonesho hayo





Thursday, August 13, 2009

Jirani Adakwa Na Madawa Akienda Afrika Kusini

Mkuu wa kitengo cha kudhibiti dawa za kulevya nchini, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Godfrey Nzowa akionesha kifurushi cha dawa za kulevya aina ya Heroin zenye uzito wa kilo 3, waandishi wa habari baada ya kukamata toka kwa raia wa Kenya Rebeka Wairimu, katika kituo kikuu cha Mabasi, Ubungo, Dar es Salaam.
Beberu Litoalo Maziwa
Mfugaji wa Mbuzi wa Kijiji cha Kilomo, Wilayani Bagamoyo, Mkoani Pwani, Abdallha Jumanne akitoa ya maelezo kwa wananchi ( hawapo pichani ) jinsi ya Dume la mbuzi lenye matiti yanayokamuliwa maziwa katika Banda la Maonesho la Halmashauri hiyo Viwanja vya Mwalimu Juluis Nyerere, Morogoro.
Picha na :www.habarileo.co.tz
TANESCO Yatangaza Mgawo Wa Umeme Dar



Na Hussein Issa

SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco) limetangaza mgao wa umeme katika jiji la Dar es Salaam kuanzia kesho hadi Agosti 28 mwaka huu.

Taarifa ya Tanesco iliyotolewa jana kwa vyombo vya habari , ilisema mgao huo utakuwepo kutokana na kazi ya kufunga transfoma katika maeneo ya Masaki na Oysterbay.

Ilisema mgao huo utuzikumba sehemu nyingine kuanzia saa 1 asubuhi mpaka saa saba mchana , wakati sehemu nyingine zikikosa umeme kuanzia saa saba mchana mpaka saa moja asubuhi.

Sehemu zitakazokumbwa na mgao huo ni pamoja na Ubalozi wa Kenya, Japan, Urusi, India, Ufaransa na Iran, Heart Institute, STANBIC, barabara za Kenyatta, Kaunda, Kinondoni (sehemu), mtaa wa Laibon na Kwale na Kinondoni Hananasifu .

Zingine ni Golden Tulip, Coco beach, Barabara ya Tumbawe , Kajificheni , Josho la mbwa, sehemu ya Kenyatta , Oysterbay hospital, Ubalozi wa South Africa, Nigeria, Oysterbay hotel, International School of Tanganyika, Karibu Hotel, Barabara ya Hill na maeneo ya jirani.

Sehemu nyingine ni pamoja na maeneo ya Baobao sehemu ya Chole Kahama mining, Bandari quarters, Nasaco flats, ATC quarters, CCBRT hospital, TIRDO
Kazi Ipo
Akiri kuwa na njama za ugaidi


DUSSELDORF

Mshukiwa mkuu wa ugaidi katika kile kinachoitwa "kesi ya Sauerland" Fritz Gelowicz amekiri makosa yake. Amesema yeye na wenzake watatu walikuwa na nia ya kuwaua askari wengi wa kimarekani waliyoko nchini Ujerumani kadri iwezekanavyo.

Mshukiwa wa pili anatarajiwa kuwasilisha ushahidi wake hii leo. Waendesha mashtaka wamesema kuwa watu wanne, wajerumani watatu na mturuki mmoja walipanga njama za kuyalipua majengo ya Marekani nchini Ujerumani kwa niaba ya kundi la kiislam liitwalo Jihad Union lenye uhusiano na kundi la kigaidi la al-Qaida.

Polisi waliwakamata watatu kati yao Septemba mwaka 2007 katika mkoa wa Sauerland.
hepi besdei ya kuzaliwa mh. pinda Jana
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimlisha keki mkewe Tunu ikiwa ni ishara yakuadhimisha siku ya kuzaliwa kwake. Alikuwa kwenye mji Mdogo wa Kibaya wialyaniKiteto akiwa katika ziara ya mkoa wa Manyara Jana. Katikati ni Mbunge waViti Maalum, Dollar Mushi.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akipokea maua kutoka kwa mkewe Tunu ikiwa nipongezi ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake . Alikuwa katika mji mdogo wa Kibaya wilayani Kiteto akienelea na ziara yake ya mkoa wa Manyara Jana




FFU wa Ngoma Africa katika Makamuzi ya hatari AFRILU Festival!
FFU wa Ngoma Africa band! wakiwa katika makamuzi ya hatari hatari! kwenye onyesho la AFRILU Festival mijin Ludwigshaven,Ujerumani, ambako onyesho hilo la ijumaa ya lililowatia kiwewe washabiki na kukubali kuwa "Bongo Dansi" la FFU wa Ngoma Africa ni virungu vya kimataifa
hakuna kulala

Ras akiongozw rigwaride la FFU



mjomba mrisho mpoto alonga

video

bofya mshale umuone na kumsikiliza mjomba

Wednesday, August 12, 2009

madame ritha atangaza 10 bora wa bongo star search
Mkurugenzi mtendaji wa Benchmark Production Madame Ritah Paulsen(kushoto) na Mkuu wa Udhamini na Mawasiliano wa Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania George Rwehumbiza(kulia)akiongea na wanahabari wakati walipotangaza kumi bora ya washiriki wa Bongo Star Search 2009.Vodacom Tanzania ni wadhamini wakuu wa shindano hilo
Washiriki wa Bongo Star Search 2009 wakiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Udhamini na Mawasiliano wa Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania George Rwehumbiza pamoja na Mkurugenzi mtendaji wa Benchmark Production Ritah Paulsen ambae ni muandaaji wa shindano hilo yakidhaminiwa na Vodacom Tanzania.