Monday, June 30, 2008

Kipanya na busara zake..

Sylivia Misss Ilala
2008...

Pichani ni Mrembo Sylvia Mashuda ndiye Miss Ilala 2008 aliyefungua pazia la kuelekea Miss Tz mwaka huu pale Raiway Gerezani sasa ni City Garden Club.She is 19 yrs old,Form vi leaver,wants to join the University...Picha kwa Msaada wa Abdallah Mrisho Salawi
Asilimia Kubwa ya Majengo Bongo
Hatari Tupu

ZAIDI ya maghorofa 100 jijini Dar es Salaam yamebainika kuwa yalijengwa kinyume cha taratibu za ujenzi,Bunge limeelezwa,ripoti iliyoundwa na Waziri Mkuu aliyejiuzulu Edward Lowassa imesema.

Maghorofa hayo ni kati ya maghorofa 505 ambayo yalikaguliwa ambapo 147 yalikutwa hayana nyaraka za ujenzi.Lowassa aliunda tume baada ya jengo la Hoteli ya Chang’ombe Village Inn, Keko,Dar es Salaam kuanguka mwaka 2006 na kuua mtu mmoja na kujeruhi wengine kadhaa. Ilidaiwa kwamba ulikuwapo ukiukwaji katika ujenzi wake.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliliambia Bunge wakatyi akifunga hotuba yake ya bajeti kuwa tume hiyo ya Lowassa, ilibaini katika ukaguzi huo,kuwa maghorofa 81 yalikutwa yamekiuka masharti ya ujenzi huku maghorofa mengine 22 wenyewe hawakupatikana na yalikuwa yamejengwa bila kuzingatia sheria za ujenzi.Panda alisema maghorofa mengi yanayojengwa Dar es Salaam yanajengwa holela bila kufuata taratibu za ujenzi,hivyo kuyafanya kuwa hatari kwa maisha ya binadamu.

Alisema kama hatua za haraka hazitachukuliwa na serikali,kuna hatari ya watu wengi kupoteza maisha kwenye maghorofa hayo ambayo yanachipuka kama uyoga katikati ya Dar es Salaam, likiwamo eneo la Kariakoo.Alisema tukio la kuporomoka kwa ghorofa kulikotokea wiki iliyopita Kisutu, Dar es Salaam, ni uzembe wa baadhi ya watendaji wakiwamo wahandisi wa manispaa husika.Alisema kutokana na taarifa hiyo ya tume,serikali inaandaa utaratibu mzuri wa utekelezaji wake kuhakikisha maghorofa yanayojengwa yanakuwa bora na yanayofuata taratibu zote za ujenzi.
Habari hii imeandaliwa na
Msimbe Lukwangule
Anna Kilango Malecela..

Mwonekano wa karibu wa Mbunge wa jimbo la Same Mashariki kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM) Mh Anna Kilango Malecela..
BongoLand II kushuka Chicago
August 5th and 20th.
BONGOLAND II is coming to Chicago...SAVE THE DATE.
The movie will premiere in the state on August 5th and August 20th.
Both shows will be at 6:15 PM. This is part of the Black Harvest International Film Festival.The venue for Premiere is Gene Siskel Film Center -
164 North Street,Chicago,IL 60601Read more about this movie at
Kibira Films Official Web site
Also see movie trailers below:
Exim yafanya Mambo
Comoro...
Exim bank imekuwa benki ya kwanza ya Tanzania kutanua huduma zake nchi za nje.Hivi karibuni benki hiyo imefungua tawi lake nchini Comoro.Tazama jinsi inavyopendeza. Picha na Mdau Bernard Rwebangira/TSN.
Mambo ya Werrason
Bongo .......


Pichani ni Mwanamuziki kutoka Kongo DRC Werrason Ngaima akiliwasha moto usiku wa kuamkia jumamosi ndani ya ukumbi wa ubungo plaza jijini Dar es Salaam nakukonga nyoyo za wadau mbalimbali waliyojitokeza kumapa shavu mwanamuziki huyo.Picha kwa hisani ya Mdau Emmanuel Herman/Ahmed Michuzi

Asante ya pombe na sigara
ni....

Asante ya kufanya urafiki na pombe na sigara,faida yake ni kicheko cha aibu ya kutosha.Tizama video (bofya hapa)wanavyomcheka kwa upumbavu wake uliotokana na kubwia pombe. Nimeidaka kwenye baraza ya Faustine' chanzo cha habari Youtube na The Sun.By Subi binti Nsipitwe

Fedha za EPA zirudishwe
Benki Kuu-Pinda..
Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akijibu hoja mbalimbali za Wabunge wakati akihitimisha mjadala wa Hotuba ya Bajeti ya ofisi yake kwenye ukumbi wa Bunge mjini Dodoma,Juni 27,2008.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu.
------
WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Mizengo Pinda,amesema mabilioni ya fedha yaliyoibwa katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA),kutoka Benki Kuu (BoT) ambayo ni taasisi ya umma lazima kurejeshwa pasipo mjadala.

Kauli ya Pinda imekuja wakati kukiwa na mjadala kuhusu nani hasa mmiliki wa fedha hizo, kufuatia Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo,kusema fedha hizo si za BoT wala serikali bali ni za wafanyabiashara.

Akifanya majumuisho ya hotuba yake mjini Dodoma ,Pinda alisema anajua shauku iliyopo ni kubwa kwani wananchi wengi wanataka kujua fedha hizo ni za nani na mwisho wake ni upi, lakini kubwa ni kwamba fedha hizo lazima zirudishwe kwa gharama yoyote.Habari na Kizitto Noya,Dodoma na Tausi Mbowe.
Rais Kikwete atua
Misri..

Waziri Mkuu wa Misri,Dk. Ahmed Nazif(Kushoto)akimkaribisha Rais Jakaya Kikwete katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sharm El Sheikh, Misri jana.Picha na Freddy Maro wa Ikulu.
--------

Rais Jakaya Kikwete,amewasili nchini Misri ambako leo atakuwa Mwenyekiti wa Kikao cha 11 cha Wakuu wa Nchi za Afrika kinachoanza katika mji wa Sharm El Sheikh.Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu leo,kikao hicho cha Wakuu wa Nchi wa AU kimetanguliwa na kikao cha siku mbili cha 16 cha kawaida cha Baraza la Utendaji la AU kilichoanza Ijumaa iliyopita chini ya uenyekiti wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard Membe.

Kikao hicho ni cha mawaziri wa Mambo ya Nje wa AU.Taarifa ya Ikulu ilisema mada kuu ya Kikao cha Wakuu wa Nchi za AU ni Maji na Usafi Wake,chini ya mada ya jumla ya juhudi za Afrika kutekeleza Maazimio la Milenia – Meeting the Millennium Development Goals (MDGs) on Water and Sanitation”.

Aidha,kikao hicho chini ya uenyekiti wa Rais Kikwete,kitapokea na kujadili Ripoti ya Kamati ya Wakuu 12 wa AU kuhusu kuanzishwa kwa Serikali ya Umoja wa Afrika.Mjadala kuhusu suala hilo umekuwa unaendelea tangu Libya ilipotoa pendekezo hilo mwaka 2005.Ripoti hiyo, itawasilishwa na Rais Kikwete mwenyewe ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo iliyokutana katika kikao chake mjini Arusha kwa siku mbili kuanzia Mei 22,mwaka huu.

Mbali na Tanzania,nchi nyingine wajumbe wa Kamati hiyo ni Ghana, Nigeria, Senegal, Libya, Misri, Botswana,Afrika Kusini,Ethiopia,Uganda,Gabon na Cameroon,ambazo zote zilihudhuria mkutano wa Arusha.Kikao cha Sharm El Sheikh pia kitajadili na kufikia uamuzi kuhusu pendekezo la kuunganishwa kwa Mahakama ya Afrika Kuhusu Haki za Binadamu na Watu wa Afrika pamoja na Mahakama ya AU.

Pia kitateua majaji wanne kati ya saba wanaowania kuwamo katika mahakama hiyo.Aidha, kitapokea na kujadili Ripoti ya Shughuli za Baraza la Amani na Usalama la AU na mjadala huo unatarajia kugusia hali ilivyo katika nchi za Comoro,Burundi,Ivory Coast,Jamhuri ya Afrika ya Kati,Somalia,Darfur (Sudan) na Zimbabwe.

Tafakari Hali
hii.......
Pichani ni vijana wadogo(watoto)wakichota maji kwenye moja ya visima vya maji ambayo si salama kama muonavyo pichani.Kisima hiki kipo maeneo ya Morogoro Road na Nelson jijini Dar es Salaam.Picha hii na mpiga picha maalum wa ThisDay

Truly inspirational.



Next Time You Think Life is Hard...Think Again!....



www.FunAndFunOnly.netwww.FunAndFunOnly.net

My name is Nick Vujicic

Their firstborn son had been born without limbs! There were no warnings or time to prepare themselves for it... The doctors were shocked and had no answers at all! There is still no medical reason why this had happened and Nick now has a Brother and Sister who were born just like any other baby.

www.FunAndFunOnly.net

www.FunAndFunOnly.net

I know that there is no such thing as luck, chance or coincidence that these 'bad' things happen in our life.

I had complete peace knowing that God won't let anything happen to us in our life unless God has a good purpose for it all

I am now twenty-three years old and have completed a Bachelor of Commerce majoring in Financial

Planningand Accounting. I am also a motivational speaker and

www.FunAndFunOnly.net www.FunAndFunOnly.net

I have a passion for reaching out to youth and keep myself available for whatever God wants me to do, and wherever He leads, I follow.

Writing several best-selling books has been one of my dreams and I hope to finish writing my first by the end of the year.

www.FunAndFunOnly.net?www.FunAndFunOnly.net

It will be called 'No Arms, No Legs, and No Worries!'

www.FunAndFunOnly.net

I believe that if you have the desire and passion to do something, and if it's God's will, you will achieve it in good time. As humans, we continually put limits on ourselves for no reason at all! What's worse is putting limits on God who can do all things. We put God in a 'box'. The awesome thing about the Power of God, is that if we want to do something for God, instead of focusing on our capability, concentrate on our availability for we know that it is God through us and we can't do anything without God

.

Once we make ourselves available for God's work, guess whose capabilities we rely on? God's!

www.FunAndFunOnly.net

Shoo ya Lady Jaydee Reading
Full Shangwee...
BAADA YA KUWARUSHA KISAWASAWA WAKAZI WA READING LADY JAYDEE AMEOMBWA NA WAPENZI WAKE KUFANYA SHOO NYINGINE MBILI CLUB AFRIQUE IJUMAA YA TAREHE 4 /O7/2008 NA JUMAMOSI YA 5/07/2008 BIRMINGHAM KWA MAELEZO ZAIDI INGIA www.bongodjs.com au www.bongouk.com
Tanzania Kilimanjaro Music
Awards 2008..

Picha juu ni wasaniii mbalimbali wakinyakua tunzo zao Tanzania Kilimanjaro music Award 2008 katika sherehe zilifofanyika Kempiski Hotel usiku wa kuamkia leo.
---------------
WASANII kumi wamechaguliwa kuingia katika shindano la kumsaka Mfalme wa hip hop hapa nchini baada ya mashabiki kupiga kura zao kutoka sehemu mbalimbali nchini.Wasanii ambao wamechaguliwa katika shindano hilo ni Kalapina wa kundin la Kikosi cha Mizinga, Chid Benz kutoka La Familia,Fid Q,Kala Jeremiah,Joe Makini,Langa,Lord Eyez kutoka Nako2Nako, Rado, Black Rhino na Profesa Jay maarufu kama Daddy.Akizungumza Mratibu wa Shindano hilo, Charles Mateso alisema lengo la kaunzisha shindano hilo ni kuleta changamoto kwa mashabiki na hata wasanii wenyewe.

"Kilichofanyika tuliendesha zoezi la kuwataka wasomaji wetu wachague ni wasanii gani wanaofaa kuingia katika shindano hilo,ambapo baada ya majumuisho ya kura zote walipatikana wasanii kumi na hao ndiyo watakaoliwania taji hilo,"alisema.Alisema mshindi wa shindano hilo atapatikana kutokana na kura za wasomaji wa ambao ndiyo watakaomchagua yule wanayemuona anafaa kuwa Ijumaa King Of Hip Hop."Litakuwa ni shindano la wazi na hakuna kumpendelea mtu,ila mashabiki ndiyo watakaoamua nani anastahili.

"“Ili kumpata mshindi wasomaji wanatakiwa kupiga kura kwa kutuma ujumbe mfupi wa maandishi kwa kuandika neno HP (acha nafasi),andika jina la msanii unayeona anastahili kushinda taji hilo na kutuma kwenda namba 15551,”alisema.Kuhusu zawadi alisema mshindi atapata zawadi kubwa itakayotangazwa hapo baadaye,huku yule aliyeshiriki kupiga kura naye akiwa katika nafasi ya kujishindia zawadi kemkem zilizoandaliwa kwa ajili yao.Picha zote kwa Hisani ya Mdau wa Blogu hii Deus Mhagale ambaye alikuwamo ukumbini.
Chacha Wangwe asimamishwa
Chadema

KAMATI Kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),imemsimamisha Makamu Mwenyekiti wa chama hicho,Chacha Wangwe (Pichani)kuendelea na wadhifa huo.
Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima Jumapili imezipata zinaeleza kuwa,uamuzi wa kumsimamisha Wangwe ulifikiwa katika kikao cha siri cha Kamati Kuu kilichofanyika jana mjini Dodoma.
Kiongozi mmoja wa CHADEMA aliyezungumza na gazeti hili kwa sharti la kutotajwa jina lake, alieleza kuwa uamuzi wa kumsimamisha Wangwe ulifikiwa kwa kauli moja na wajumbe wate wa Kamati Kuu isipokuwa Wangwe ambaye aliupinga.
Alisema, Wangwe amesimamishwa baada ya kubainika kuwa na makosa ya kukigawa chama katika makundi na kusababisha kuwepo kwa mgawanyiko mkubwa katika ofisi za makao makuu.
Habari zaidi zilieleza kuwa,Wangwe amepinga uamuzi huo na anatarajiwa kuanza ziara ya mikoani yenye lengo la kuwaeleza wanachama kilichasababisha kufikiwa kwa hali hiyo.kwa mengi zaidi bofya Hapa

Kigoma..
Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akisalimaina na Viongozi wa Dini wa mkoa wa Kigoma baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Kigoma kwa ziara ya sikumbili mkoani humo,Juni 29,2008.Kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Kigoma,Kanali Joseph Simbakalia.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
Tanzanite Fc,Atlanta wajitolea kulipa
Jezi ya Mchezaji wa
Taifa Stars..
--------------------
Habari yako,
pole na shughuli nzito ya kuwakilisha jamii.Sisi Vijana wa Tanzanite fc Ya Atlanta Ga tunasikitika na habari tuliyosoma juu ya mchezaji wetu aliyewakilisha timu yetu ya taifa huko Cameroon kwa kuadhibiwa kwa kulipia jezi ya timu ya taifa aliyobadilishana na mchezaji mwenzie wa Cameroon(Etoo)tumeona kwamba ni swala la aibu kwa chama cha soka cha Tanzania kumdai mchezeji huyo hasa ukizingitia mchango wake kwa Taifa.
Sisi Tanzanite fc tungependa kujitolea kulipa deni hilo la huyo mchezaji. Je ni utaratibu gani tuutumie kuwakilisha mchango huo, na je ni kiasi gani?Tunatanguliza shukrani zetu kwa msaada wako kutufanikishia swala hili.
Wako
Tanzanite fcAtlanta,GA.
USA
Naibu Meya Dar atangaza
kujiuzulu...


Meya wa Manispaa ya Ilala Dar es Salaam, Bw.Mohamed Yakubu (Pichani),ametangaza kujiuzulu nafasi aliyonayo kwa madai kuwa anataka kuachia wengine washike nafasi hiyo na yeye kuelekeza nguvu zake katika kujiendeleza kielimu. Taarifa za kujiuzulu kwa Bw.Yakubu zililifikia Majira Jumapili Dar es Salaam jana kutoka kwa chanzo cha kuaminika ambacho kieleza sababu za kujiuzulu kwake.


Taarifa za kujiuzulu kwa Bw.Yakubu zililifikia Majira Jumapili Dar es Salaam jana kutoka kwa chanzo cha kuaminika ambacho kieleza sababu za kujiuzulu kwake. Akizungumza kwa njia ya simu jana Bw.Yakubu alisema ni kweli yupo katika harakati za kujiuzulu nafasi ya Unaibu Meya wa Manispaa hiyo ingawa bado hajaandika barua rasmi kwa uongozi wake wa juu."Bado sijaandika baarua rasmi ya kujiuzulu nafasi hiyo lakini natarajia kuandika barua siku yoyote kuanzia kesho kuujulisha uongozi wangu wa juu akiwemo Meya wa Manispaa ya Ilala Alhaj Abuu Jumaa," alisema Bw.Yakubu.

Alisema kujiuzulu ni uamuzi mzito lakini kwa upande wake ameamua kufanya hivyo kwakuwa anatarajia kuanza masomo ya Utawala katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam sehemu ya Mlimani. Alisema pindi atakapoanza masomo yake itakuwa vigumu kwake kujihusisha moja kwa moja kutoa huduma kwa wananchi akiwa katika nafasi ya Naibu Meya.Habari na Na Said Mwishehe

Saturday, June 28, 2008

Ushauri Wa Kipanya
" E Bwana , Tusilaumiane B'dae, N'na Jiwe Hapa!"
Da' Subi: His Name Is Nelson Mandela!
Inaelekea kuna mtu alifanya uandishi kutumia 'auto complete' wakati wa kazi halafu akalibandika tu alimradi...
Afadhali CNN wameondoa na kurekebisha maana ingekuwa si njema.
Dah, akikosewa jina Mandela sisi akina Chipiliro wa Akapungwamchanye sijui itakuwaje.
Tizama kipande cha picha nimekiambatanisha hapa.
iliyokuwa klabu ya relwe gerezani ilivyo sasa
sehemu za uani (juu) na barazani pa iliyokuwa klabu ya relwe gerezani inavyoonekana leo. itapokamilika na kufunguliwa itajulikana kama city garden club mmiliki akiwa mdau yule yule wa paradise beach resort ya bagamoyo, city garden na dar es salaam international conference centre na pia city garden restaurant ambayo zamani ni cosy cafe usoni pa mbowe hotel ama billicanas kwa sasa
ma DJ veterani
dj chris phabby the lover (shoto) akiwa na dj ngomeley. hawa ni baadhi ya watoa burudani enzi hizo za 'maiko jekson njoo, sitaaaaaki, kama hutaki nenda...' nina imani bonny luv atawawakilisha vyema kwenye oldskul party huko columbus siku ya siku ikiwadia. dj luke upo hapo? unakumbuka dy chris phabby alivyokuwa anamwaga lazi ymca na dj ngomeley alivykuwa kule rungwe oceanic kwa mzee mwakitwange??
NMB yazindua huduma za kulipia LUKU kwa ATM

Mkurugenzi Mtendaji wa NMB Ben Christiaanse akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Dk. .Idrisa Rashid wakati wa uzinduzi wa NMB ATM LUKU Recharge.

Siku ya Tarehe 25 June 2008, NMB imeweka historia mpya katika utoaji wa huduma za kibenki kwa kuanzisha huduma ya kununua LUKU kwenye ATM za NMB yaani NMB LUKU RECHARGE bila gharama yeyote ya ziada . Huduma hii inaenda sambamba na ukuaji wa uwekaji wa ATM nchi nzima.

NMB ilikuwa ni benki ya kwanza kutoa huduma za kuchukua fedha kwenye ATM bila gharama.Hadi sasa NMB ina ongoza kwa kuwa na ATM nyingi kuliko benki nyingine, hadi sasa tayari ina mashine za ATM 115 na ifikapo mwisho wa mwaka huu itakuwa na ATM 200 nchi nzima.
Chini ni bosi wa masoko wa NMB Imani Kajura (shoto) akipeana mikono na mmoja wa wateja wa kwanza wa Tanesco waliotumia huduma hiyo mara tu baada ya kuzinduliwa
Shairi kwa kumkumbuka Amina Chifupa

Bado tunakukumbuka

Mwaka sasa umepita, bado tunakukumbuka,
Machozi hatujafuta, bado tunahuzunika,
Jina bado twaliita, kumbe ulishatutoka,
Bado tunakukumbuka, rafiki yetu Amina.


Ni vigumu kuamini, kuwa ilishatokea,
Machungu tele moyoni,vigumu kuyazowea,
Haupo tena duniani, mbali umeelekea,
Bado tunakukumbuka, rafiki yetu Amina.


Ni kama utani vile, ua letu kunyauka,
Nakumbuka siku ile, kichwani haitotoka,
Umekwenda zako kule, mwisho wako ‘ulipofika,
Bado tunakukumbuka, rafiki yetu Amina.


Amina mpiganaji, mahiri wetu vijana,
Nasi tulikutaraji, ‘ungetusaidia sana,
Mambo yetu kuyahoji, majibu kupatikana,
Bado tunakukumbuka, rafiki yetu Amina.


Uliacha changamoto, kwenye timu ya taifa,
Sasa imepamba moto, yacheza kwa maarifa,
Na sasa tunayo ndoto, itat’uongezea sifa,
Bado tunakukumbuka, rafiki yetu Amina.


Bunge uliloliacha, sasa kumepambazuka,
Kwa hakika kumekucha, hoja zinajadilika,
Kwa mafisadi kwachacha, kwao moto unawaka,
Bado tunakukumbuka, rafiki yetu Amina.


Ila vita ya madawa, bado inasuasua,
Ingawa wanaelewa, moyoni ‘ilikusumbua,
Dhati kwao haijawa, bado hawajatatua,
Bado tunakukumbuka, rafiki yetu Amina.


Amina dada Amina,rafiki yetu wa kweli,
Kama ingewezekana, kulitenda jambo hili,
Basi tungeomba sana, uturejee kimwili,
Bado tunakukumbuka, rafiki yetu Amina.


Kimwili haupo nasi, kiroho tupo pamoja,
Ni kweli tunakumiss, tutakuwona siku moja,
Familia yakumiss, Mungu aipe faraja,
Bado tunakukumbuka, rafiki yetu Amina.


Naweka kalamu chini, bado sisi twakupenda,
Upumzike kwa amani, mahali ulipokwenda,
Mahala pema peponi, malaika akulinde,
BADO TUNAKUKUMBUKA, RAFIKI YETU AMINA.




Ewe mdau Fadhili, asante we kwa shairi,
Nakuomba tafadhali, uniweke mstari,
usio mshahadhali, katika hili shauri,
Amina twamkumbuka, masikini na tajiri.


Twamkumbuka Amina, tajiri na masikini,
Na la kufanya hatuna, aliyopanga manani,
Anatajwa kila kona, kwamba awekwe peponi,
Amina twamkumbuka, masikini na tajiri.


Na siku zaenda mbio, kama vile ni utani,
Toka saa za machweo, hadi muda wa jioni,
Twaendeleza vilio, wapi Amina jamani,
Amina twamkumbuka, masikini na tajiri.
Hakika sikunuia, kukushukushuru globuni,
Mradi imetokea, acha na mie nighani,
Uchungu umegusia, ulotukaa moyoni,
Amina twamkumbuka, masikini na tajiri.


Kuna waliosahau, mwezi huu alitutoka,
Asante kwa yako mbiu, muda huu muafaka,
Ye si wa kumsahau, watu wa kila tabaka,
Amina twamkumbuka, masikini na tajiri.


Globu yako e fadhili, nimepita kwa yakini,
sikuona ufedhuli, ulojaa duniani,
Haki utafika mbali, kama si leo mwakani,
Amina twamkumbuka, masikini na tajiri.
Kaditama ninaomba, leo nikomee hapa,
Nikizidi kukuomba, daima usiwe kapa,
Endelea kaza kamba, usije ishia hapa,
Amina twamkumbuka, masikini na tajiri.
Salamu zangu za mwisho, mlio kama Fadhili,
Twahitaji burudish0, katika hapa pahali,
Kama hakuna mipasho, hapa ni penu mahali,
Amina twamkumbuka,masikini na tajiri.
- Kadidi-



warembo kukosha magari kwa hisani

Bonanza hili litafanyika leaders club Julai 5, 2008 ambapo warembo walioshiriki miss Tanzania kuanzia mwaka 1994 hadi sasa.

Warembo hao wataosha magari ya watu mbalimbali kwa ajili ya kutunisha mfuko wa sickle cell foundation Tanzania.

Zoezi hili litadhaminiwa na Tigo, Le Grande Casino, Clouds 88.4 FM, Fleet & Fuel Technologies, Redds PremiumCold
hakuna kabila la wachagga
Kadidi na wadau,
Blog hii ya jamii kwa sasa inaendelea kujadili mada nzito ambazo zinawasaidia wadau mbalimbali katika maisha yao ya kila siku.
Mimi leo naleta mada inayohusu kabila liitwalo 'Wachagga' na kama kweli lipo kihalani. Kwa kuanza naomba wasomi, wana zuoni, na hao waitwao wachagga wawe ndo wachangiaji wakuu katika maelezo nitakayotoa hapa chini.
Ni ukweli kwamba kabila lolote linaundwa na watu ambao wanazungumza lugha moja, na kuwa na mila na desturi zinazofanana.
Kwa kimombo "A CERTAIN TRIBE IS MADE UP OF PEOPLE WHO SPEAK THE SAME LANGUAGE, AND ALSO SHARE THE SAME CULTURES AND TRADITIONS.'
Sasa kwa hawa wanaojiita wachaga waishio mkoani Kilimanjaro wengi wao hawazungumzi lugha moja na mila na desturi zao ni tofauti.
Mfano ni kwamba Warombo wana lugha yao na tamaduni zao tofauti. Hali ni kama hiyo hiyo kwa watu wa Vunjo(watokao Mamba, Mwika, Marangu, Kilema na Kirua, Old Moshi, Uru, Kibosho, Machame, Lyamungo, na Sanya Juu).
Wote hawa wana mila, desturi, na tamaduni zao TOFAUTI. Sasa ni kwa nini wote hawa kwa wingi wao waitwe 'WACHAGGA?'.
Makabila mengine nchini kila moja yana lugha moja, ikiwa ni pamoja na desturi na mila zisizotofautiana miongoni mwa watu.Kwa sasa najitahidi naandika kitabu kuonyesha kuwa hakuna kabila liitwalo
WACHAGGA, bali kuna warombo, wakibosho, wamarangu, wamachame, wauru na wa old moshi. Wadau nipo sawa? Naomba michango...
DEO MUSHI
DAILY NEWS - ARUSHA OFFICE
dar events this weekend
SUNDAY 29/06/2008
Moevenpick & Partners
presents
EURO CUP FINAL @ MOEVENPICK ROYAL PALM HOTEL
"GERMANY VS. SPAIN"
Expected emotions and loads of fun in perspective…
get ready to kick in! -
Event format –
Timing: 05.00pm till 12.00am
Entertainment: Bora Bora Live Band
Activity: Business card raffle and trip to Europe to win!
F&B: Welcome drink upon arrival / Free aromatic BBQ / Cash Bar
Entrance fee: Tsh35.000/-
Come and celebrate with us the most exciting night of the cup!
Spoilt your guests and friends in purchasing tickets for the final!
HURRY UP! TICKETS AVAILABLE NOW!!!
@ MOEVENPICK ROYAL PALM HOTELLOBBY AREA,
NEXT TO BAKERY SHOP
FROM MONDAY TO SATURDAY
09.00AM – 01.00PM02.00PM -
06.00PM SUNDAY02.00PM – 10.00PM
EMPOWERED BY: MOEVENPICK ROYAL PALM HOTEL
/DSTV/COCA-COLA/KLM ROYAL DUTCH AIRLINES
/CASTLE/RED PROMOTIONS LTD
mtumishi mwakasege kutua dallas septemba

Ndugu, Jamaa na Marafiki,


Tunapenda kuwakaribisha kwenye semina ya neno la Mungu itakayohudumiwa na watumishi wa Mungu CHRISTOPHER & DIANA MWAKASEGE toka Tanzania.


Semina hii ya kipekee na yenye ujumbe maalum kwa kila mtu itafanyika Dallas,Texas USA September 12 hadi 14 2008.


Mungu amekuwa akiwatumia hawa watumishi ndani na nje ya nchi kwa Upako na wengi wamefunguliwa,kuponywa na kutiwa moyo kupitia huduma hii.


Unaweza kujionea yale Mungu anayotenda kwenye mtandao huu
WWW.MWAKASEGE.ORG Maelekezo zaidi kuhusiana na sehemu itakapofanyika pamoja na utaratibu mzima vitafuata.

Tafadhali mtaarifu mwingine juu ya Semina ya Baraka!


Kwa maelezo zaidi unaweza kuwasiliana kwa njia ya email :- KULA.MANA@YAHOO.COM


au simu kama zifuatazo:-

Dallas: 21-440-9674 //469-233-6627 // 214-554-7381

Chicago: 312-823-5878

Atlanta:404-245-5339 //678-982-2113

Boston: 978-726-2227Ohio:214-505-8514

Alabama: 402-770-6376

Minnesota:651-263-7831//763-238-1617// 952-564-8298

Penginepo:651-334-0163

Timu ya Maandalizi,

Mungu Awabariki....!!
tigo yafanya kweli sabasaba 2008

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Biashara ya nje inayoandaa Maonyesho ya Biashara ya SabaSaba Mh. Ramadhani Khalfan akikata utepe lango kuu katika uwanja wa mwalim J K Nyere mara baada ya kampuni ya simu ya Tigo kukabidhi maeneo ya kimvuli cha kudumu yaliyojengwa na Tigo kwa ajili ya kuwakinga jua na mvua waalikwa na wageni watakaotembea viwanjani hapo wakati wa maonyeso kuanzia Jumamosi hii. Shoto ni bosi wa Masoko wa Tigo Kelvin Twissa.



Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa maonesho ya 32 ya sabasaba Julai 1, 2008, ambapo kutakuwa na maonesho ya nchi 27, wizara 9, idara 38 na serikali, kampuni za bongo 650 pamoja na wadau wa biashara ndogondogo 60, wakiwamo machinga ambao wanashiriki kwa mara ya kwanza mwaka huu.

Daily News na HabariLeo nao watakuwepo kufanya kile walichofanya wakati wa mkutano wa Sullivan A-taun kwa maonesho ya mapicha na shughuli za gazeti hilo mama la magazeti nchini ambalo limeendeleza libeneke kwa miaka 75 sasa.

Tigo ndio kampuni rasmi ya mawasiliano katika maonesho haya na tayari imeanda shughuli kibao na zawadi kedekede kwenye banda lake
if jongwe were