Saturday, January 3, 2009

mgonja aunganishwa na akina mramba na yona



Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam, jana imemuunganisha aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Grey Mgonja, katika kesi ya watuhumiwa wengine wa ufisadi, Basil Pesambili Mramba na Daniel Yona.

Wote hawa wanakabiliwa na tuhuma za kutumia vibaya madaraka yao na kulisababishia taifa hasara ya takribani bilioni 11.Hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Hezron Mwankenja alifikia hatua hiyo kufuatia ombi la upande wa utetezi katika kesi ya Mgonja unaoongozwa na Profesa Leonard Shaidi, kuiomba mahakama hiyo kumuunganisha mteja wake na akina Mramba na Yona kwa kile alichodaiwa kuwa kesi hizo zinafanana.

Pichani aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba (kulia) akiteta jambo na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Daniel Yona (katikati) wakati walipokuwa mahakamani, mapema mchana hii leo Kushoto ni Grey Mgonja.

No comments: