Thursday, January 29, 2009

nakuja na mambo mapya-Steve Nyerere


Steve Nyerere akiwa kwenye maandalizi makubwa ya kipindi chake ambacho kitahusisha mchakato mzima unaoizunguka jamii pamoja na wageni waalikwa ambao watakuwa wakichangia mada hizo kwa namna moja ama nyingine

Shoto ni Boss wa HATMAN PRODUCTIONS pamoja na mwanamuziki wa FM Academia Patchou Mwamba wakivutiwa na uandaaji wa kipindi cha Steve Nyerere talk show kitakachoanza kurushwa hewani mwezi ujao na televisheni ya TBC 1 jijini Dar

Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia kwa makini maandalizi makubwa ya kipindi cha Steve Nyerere talk show

Steve akimuigiza Rais Jakaya Kikwete wakati wa maandalizi ya kipindi chake

Msanii mchekeshaji na muigizaji wa sauti mbalimbali za watu maarufu ajulikanae kwa jina la Steve Nyerere akimuigiza Rais JK katika moja ya hotuba zake,hayo ni moja ya maandalizi makubwa na ya kufa mtu ya utengenezaji wa kipindi chake kitakachoitwa Steve Nyerere Talk Show kitakachokuwa kinarushwa na televisheni ya TBC hapa jijini Dar.Kipindi hicho kinachorekodiwa na kampuni ya HATMAN PRODUCTIONS kinatarajiwa kuanza kurushwa hewani mwezi ujao,haya wadau kaeni mkao wa kula mambo mapya yanakuja TBC.

NB: Ukimuhitaji Steve Nyerere katika shughuli zako mbalimbali wala usisite bofya namba hii 0715 782424 na utasikilizwa na kujibiwa haraka.

No comments: