Wednesday, January 28, 2009

bongo kutamu
maeneo ya mwanga


Blaza Kadidi, na mwenzio Kamanda Kombe

Nimekutumia hii picha niliyoipiga hivi punde, ili na wadau wengine wajionee Bongo isivyo tambarare.

Ni wiki mbili tu zimepita tangu ajali itokee huko Tanga kwa basi kuligonga nyuma lori lililokuwa limeharibika, pasi kuwa na vielelezo vyovyote kuwa limesimama kwa ubovu, na wala hapakuwa na reflectors nyuma ya lori hilo.

Hebu tazama hili gari ya takataka, hapa niliibamba ikikata kona, kutoka barabara ya M/nyamala kuingia Kawawa, indiketa zake hazifanyi kazi, taa za nyuma hata moja haiwaki, kibao cha namba hakipo, na huu wavu waliozuia nao uchafu unavujisha kidogo kidogo, thus uchafu ulikuw aunadondoka barabarani. Pia tairi zake kipara wakati limebeba mzigo mzito namna hii.

Swali; Hii inamaanisha traffic hawalioni? Au mnaliona na huwenda hawaruhusiwi kulikamata? au huwenda ndio linavyotakiwa kuwa kiuchafuuchafu?, au hili lori liue watanzania wangapi ndio mpate pa kuanzia kuchukua hatua ili tuione mnafachapa kazi?

Imagine gari kama hilo mdau linapata breakdown usiku, alafu unakuja nyuma yake itakuwaje? Natumai kama mhishimiwa fulani angekuwa na maono kuwa baada ya siku kadhaa gari yake ingejibamiza hapo nyuma ya hii lori, maamuzi yake ya leo yangekuwa tofauti.Au angekuwa na maono kuwa school bus alilopanda mtoto wake italivaa lori hili kwa nyuma, angechukua hatua flani leo. Kwakuwa haya yoote hatuwezi kuwajua ni bora kuchukua hatua leo.

Mdau MG
( Koplo wa polisi jamii)

No comments: