Wednesday, March 26, 2008

Hiyo Ni Mwananyamala kwa Ndugu yetu A.....a !!


mjadala pepe

Amini usiamini majadiliano tunayofanya kwenye makundi pepe na kupitia blogu mbalimbali, maoni endelevu yanayoandikwa humu yanawafikia watu kadhaa na pale inapowezekana hatua mahsusi zimechukuliwa.

Picha inayoonekana hapo amenitumia rafiki yangu mmoja aliyoipiga jana eneo la Mwananyamala baada ya mvua kunyesha. Nomba kuifikisha kwa wadau, tafadhali tunaomba mchango katika hili.

Tushirikishane mawazo na suluhisho la matatizo madogo madogo kama haya ambayo tukiyazuia ni rahisi sana kuepuka magonjwa ya mlipuko na kwa hivyo angalao kupunguza idadi ya wagonjwa wa mara kwa mara ambapo kukosekana nguvu kazi yao huchangia pia kupungua kwa uzalishaji na ujenzi wa nchi.

Tujadiliane tafadhali. Hii ndiyo faida ya elimu kwa njia ya mtandao wa intaneti hata ikiwa inawafikia wachache, hao hao wachache ndiyo wanaohusika na kutoa chachu na maelezo ya kimaendeleo.

Elimu muafaka ni kito cha thamani!

Mdau Subi

No comments: