Friday, March 28, 2008

Mh Zitto Kabwe afichua Siri...


NCHI wahisani zimetishia kutochangia bajeti ya nchi ya mwaka 2008/2009 kama serikali haitachukua hatua kali dhidi ya mafisadi waliochota mabilioni ya shilingi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) na mkataba wa kinyonyaji wa kufua umeme wa dharura kati ya serikali na Kampuni ya kitapeli ya Richmond.
Hayo yalibainishwa jana na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema) wakati akichangia katika kikao cha mwongozo wa kutayarisha mipango na bajeti ya serikali kwa kipindi cha mwaka 2008/2009 kwenye Ukumbi wa DICC, Dar es Salaam, kauli ambayo ilimlazimisha Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo kukiri.

No comments: