Tuesday, September 23, 2008

latoya atolewa big brother 111


Mshiriki wa Tanzania kwenye Shindano la Big Brother III, Latoya Lyakurwa amedaiwa kuponzwa na vitu vitatu ndani ya mchuano huo unaoendelea nchini Afrika Kusini.

Kitendo chake cha ‘kukandamiza malavidavi’ na Ricco wa Angola ni pointi ya kwanza ambayo ilimuondolea sifa ya kuendelea kubaki ndani ya mjengo.

Pointi ya pili ni pale aliponaswa na kamera akila denda na Moris wa Uganda, wakati huo huo mara kadhaa akawa anachojoa mbele ya wenzake, tabia ambayo haiendani na maadili ya Mtanzania na Muafrika kwa ujumla.

Kufuatia hali hiyo, Latoya atatakiwa kuwaomba radhi Watanzania kutokana na kuchafua ‘hali ya hewa’ ndani BBA ambayo ilisafishwa vizuri na Mwisho Mwampamba mwaka 2003 na Richard Bezuidenhout mwaka jana.

Pamoja na hivyo Jumamosi iliyopita, Latoya alionesha uzalendo wa kutosha kwa kuzifagilia baadhi ya kazi za wasanii, Hamisi Mwinjuma ‘Mwana FA’ na Joseph Haule ‘Prof. Jizze’ ambazo zilionesha kumpagawisha kwa sana.

chumba maalum walimowekwa na Tawana wa Botswana wakati wakisubiri mmoja wao kutoka, akiweka CD zenye nyimbo za wasanii hao na kucheza kwa hisia.

Mbongo huyo ambaye kwa upande mwingine alionekana kama amekumbuka nyumbani alianza kupagawa na ngoma za Mwana FA, ikiwemo inayotamba hivi sasa, ‘Bado Nipo nipo’, kisha akabadilisha na kuweka CD yenye nyimbo za Profesa Jay, kitu ambacho kilimfanya apandishe mzuka zaidi wa kucheza na kuimba, hasa aliposikia kazi kama ‘Hapo Vipi’, ‘Ndivyo sivyo’ na ‘Nang’atuka’.

Pamoja na mabaya yote aliyoyafanya mjengoni humo, safu hii inampa ‘big up’ za kutosha Latoya kwa kuonesha uzalendo huo wa kuzifagilia na kuzipa promo kazi za Wabongo wenzie. Wakati huo huo, mshiriki kutoka Kenya, Sheila anaendelea kupeta kimapenzi na Takondwa ‘TK’, kitendo kinachowafanya washiriki wengine wakae wakinong’ona juu yao.

Habari kwa hisani ya abdlahmrisho.blogspot.com

No comments: