Wednesday, September 24, 2008

Bomoa Bomoa Magomeni...




Familia sita zimekosa sehemu ya kuishi baada ya watu wanaodaiwa kununua nyumba ya urithi ya watoto zaidi ya 10 wa marehemu mzee Yussuf Mbonde iliyoko magomeni mwembechai kubomoa nyumba hiyo kwa kutumia greda huku wakilindwa na vijana wa kukodi maarufu wanaojulikana kama mabaunsa pamoja na usimamizi wa polisi waliokuwa na silaha.

Bomoa bomoa hiyo ilitokea juzi majira ya saa 9.00 alasiri baada ya uvamizi huo kutokea kusambaratisha nyumba na vitu vyote vilivyokuwemo ndani.

Pichani juu ni baadhi ya wanafamilia hao wakilia kwa uchungu baada ya kuona nyumba yao ikisambaratishwa vibaya sana na vitu vyao vyote vya ndani vikiwemo...picha kwa hisani ya mzee wa mshitu.

No comments: