Friday, September 19, 2008

JK amfariji mpiganaji athumani hamisi muhimbili
JK jioni hii alikuwa miongoni mwa ndugu, jamaa na marafiki waliofika hospitali ya muhimbili kitengo cha mifupa kumfariji mpiganaji athumani hamisi aliyelazwa hapo kufuatia ajali ya gari aliyopata wiki iliyopita huko kibiti, wilayani rufiji, mkoa wa pwani alikoenda kikazi
JK akiongea na athumani hamisi huku mchumba wake aliyewasili jana toka marekani akiwa karibu
baada ya kumjulia hali athumani hamisi, JK alipita kwa wagonjwa wengine na kuwafariji. hapa anamfarji david kasembe wa mamlaka ya bandari ambaye pia alipata ajali siku moja na athumani, na wote wako wodi moja hapo MOI
supa modo happiness magesse na mkuu wa itifaki wa kamati ya miss tanzania albert makoye nao walikuwepo kumpa pole mpiganaji athumani hamisi
mzee hamisi msengi, baba mzazi wa mpiganaji athumani hamisi akimfariji mwanae leo.

hali ya mgonjwa inaendelea vizuri ingawa anahitaji matibabu zaidi nje ya nchi. habari zimeingia sasa hivi zinasema serikali imeamua kumpeleka akatibiwe nje na taratibu zote zimetimia. huenda akasarirshwa kesho ama keshokutwa, ila nchi atayokwenda itajulikana kesho. athumani amejeruhiwa mfupa wa mgongo na shingoni

tunamuombea mpiganaji mwenzetu nafuu ya haraka

No comments: