Saturday, December 20, 2008

Mrocky Mrocky atunukiwa
Nishani...


Mpiga picha wa Daily News,Bw Mroki Mroki(Kushoto) ametunukiwa nishani ya Anjouan, kutokana a mchango wake katika kuhabarisha jamii wakati wa mapambano ya kumng'oa kiongozi wa waasi nchini Comoro na Waziri wa Ushirikiano wa Kimataifa Nchini Mheshimiwa Bernard Membe.

Ndani ya nchi yetu ya Tanzania,Bw Mroki amekuwa ni mmoja wa wapiga picha walio mstari wa mbele katika kutuhabarisha kuhusu matukio mbali mbali yanayohusu maisha ya kila siku ya Mtanzania.Kutafuta kwake habari kumemfanya mara nyingine apate misukosuko katika kazi hii.Nakumbuka mara ya mwisho ni ile tafrani iliyotokea katika mahafali ya Chuo Kikuu Huria.
kwa niaba wa wadau wote wa blog hii tunapenda kumpongeza Mdau Mrocky Mrocky

No comments: