Saturday, December 20, 2008

Blogu Ya Nyimbo Za Dini
Baada ya kuchoka kukimbia huku na huko mtandaoni kusaka nyimbo za dini hasa katika kipindi hiki cha kuelekea sikukuu za Krismasi na mwaka mpya (2009), nimeamua kuanza kuzikusanya na kuziweka nyimbo mbalimbali za dini katika blogu hii: nyimbozadini.blogspot.com Nachukua nafasi hii basi kuwakaribisha wadau wote wanaopenda kusikiliza nyimbo za dini kuitembelea blogu hiyo. Ni lazima niseme pia kwamba ndiyo tu nimeianzisha blogu hii na kutokana na pilipilika kuwa nyingi sijapata muda hasa wa kuishughulikia ipasavyo na kwa hivyo uchanga wake unaonekana wazi. Maoni ya jinsi ya kuiendeleza zaidi yanakaribishwa. Blogu yangu ya kiuchambuzi wa kiundani kabisa wa masuala mbalimbali yanayoihusu nchi yetu inakuja hivi karibuni.

Natanguliza shukrani zangu

Mwalimu Masangu Matondo Nzuzullima

No comments: