Thursday, October 23, 2008

wasanii wa bongofleva watinga tuzo za kisima awards

‘Binti Kiziwi’ wa Z-Anto (juu pichani) nao umechaguliwa kuwa ni miongoni kati ya nyimbo ambazo zinagombea nafasi ya wimbo bora kutoka Tanzania katika tuzo za kisima Awards, zinazotarajiwa kufanyika nchini Kenya tarehe 29 Novemba, ili kumfanya Z-Anto alinyakue jituzo hilo utatakiwa kutuma ujumbe mfupi kwa njia ya simu kwa kuandika 25E kisha unatuma kwenda kwenye namba 4142.Kumchagua Z-Anto ni kutoa mchango kwenye sanaa ya Tanzania.Mungu Ibariki Tanzania


Wadau toeni sapot yenu ya kutosha kwa kumchagua Msanii Cassim (pichani kulia) ,kwani amechaguliwa kushiriki katika tuzo za kisima Awards zinazotarajiwa kufanyika nchini Kenya novemba 29 mwaka huu.


Ili kumpa ushindi msanii wetu Cassim utakaomuwezesha kuchukua tuzo ya wimbo bora kutoka Tanzania na singo yake ‘Haiwezekani’ ambayo ndio imeshiriki katika kinyang’nyiro hicho, unatakiwa kuandika namba 22B kisha unaituma kwenda kwenye namba 4142.

Kumchagua Cassim ni kutoa mchango kwenye sanaa ya Tanzania.
Mungu Ibariki Tanzania.

Mungua Ibarikia Afrika

No comments: