hivyo ndivyo fiesta ilivyofana dodoma
Mwana-Fa akizikonga nyoyo za wakazi wa Dodoma jana jioni kwenye tamasha la fiesta jirambe,ambapo maelfu ya mkoa huo walijitokeza kujionea live bila chenga wasanii wawapendao .Washikaji baada ya kumaliza Dodoma, libeneke linaendelezwa jijini Mwanza .a.k.a The Rock City,ambako fiesta imepangwa kufanyika usiku wa jumamosi a.k.a Novemba1 katika ukumbi wa Yatch Club na Jumapili ngoma inahamishiwa uwanjani CCM kirumba huko ndiyo washabiki na wapenzi wa fiesta wanapewa nafasi kubwa ya kujiramba kwa nafasi kabisa.Si ya kukosa babake,yaani full mizuka
Tamasha la fiesta jirambe 2008 jana mchana lilikuwa pande ya wakazi wa Dodoma,eebwanae ilikuwa ni noma,wakazi wa Dodoma wanajua kujiramba ile kisawa sawa,jana jirambe ilikuwa inafanyika ndani ya uwanja wa mpira wa Jamhuri,wasanii wa chini ya handaki walianza kupanda jukwaani kuanzia majira ya saa sita na ushee hivi na baadaye wakongwe waakaanza kuangusha libeneke la bandika bandua,palikuwa hapatoshi uwanjani hapo.Pichani ndio kama uonavyo umati wa wakazi wa Dodoma ulivyoamua kujiramba kwa staili ya aina yake.
No comments:
Post a Comment