Tuesday, October 28, 2008

hivyo ndivyo fiesta ilivyofana dodoma

Nyuma ya jukwaa pia kushoo love kulikuwepo na kubadilishana mawazo kimtindo kama hivi kwa kutosha kabisa.Toka shoto ni albert Mangwea, Mhariri wa gazeti la Mwananchi starehe Henry Mdimu a.k.a Zee la Nyeti pamaja na Mwana-FA
Mh Temba kutoka kundi la wanaume TMK akiwakilisha vilivyo jukwaani,

Baadhi yao walijiramba mpaka kupitiliza kama uoanavyo pichani,jamaa alijiramba mpaka ile akhaaa! si umecheki kopo zake mbili pembeni za naniihiiiii hana hamau nazo tena


Prof Jay nae kama kawa na umahiri wake wa kuieteka hadhira vilivyo ndani ya uwanja wa Jamuhuri Dodoma jana jioni




Mwana-Fa akizikonga nyoyo za wakazi wa Dodoma jana jioni kwenye tamasha la fiesta jirambe,ambapo maelfu ya mkoa huo walijitokeza kujionea live bila chenga wasanii wawapendao .Washikaji baada ya kumaliza Dodoma, libeneke linaendelezwa jijini Mwanza .a.k.a The Rock City,ambako fiesta imepangwa kufanyika usiku wa jumamosi a.k.a Novemba1 katika ukumbi wa Yatch Club na Jumapili ngoma inahamishiwa uwanjani CCM kirumba huko ndiyo washabiki na wapenzi wa fiesta wanapewa nafasi kubwa ya kujiramba kwa nafasi kabisa.Si ya kukosa babake,yaani full mizuka

Msanii kutoka nyumba ya vipaji (THT) Mwasiti akilivua pendo mbele ya umati mkubwa wa wakazi wa Dodoma waliofika jana jioni kwenye tamasha la fiesta
Wakazi wa Dom walijitokeza kwa wingi kuunga mkono tamasha la fiesta jirambe lililofanyika jana mchana ndani ya uwanja wa jamhuri

Jay Mo akighani huku umati wa wakazi wa Dom ukimsilikiza kwa makini


Ukipenda muite brazamen au Mr Misifa Dully Sykes akionesha umahiri wake wa kucheza na maik mbele ya umati wa wakazi wa Dom hiyo jana jioni



Wasanii kutoka nyumba yenye vipaji a.k.a THT wakiwa jukwaani wakiwakuna wakazi wa Dodoma jana mchana kwenye tamasha la fiesta jirambe lililofanyika kwenye uwanja wa mpira wa Jamhuri,ambao maelfu ya wakazi wa mji huo walijiachia vya kutosha



Vibweka kama hivi vya kujiachia kutoka juu ya jukwaa vilikuwepo vya kutosha tu,na watu walipata rahaaa

Ilikuwa ni full kujiramba,mayowe,shangwe zilipata mahala pake,kila shabiki alieonekana kukunwa vilivyo na msanii yeyote yule hakusita kupiga winja na kuinua mikono hewani



Tamasha la fiesta jirambe 2008 jana mchana lilikuwa pande ya wakazi wa Dodoma,eebwanae ilikuwa ni noma,wakazi wa Dodoma wanajua kujiramba ile kisawa sawa,jana jirambe ilikuwa inafanyika ndani ya uwanja wa mpira wa Jamhuri,wasanii wa chini ya handaki walianza kupanda jukwaani kuanzia majira ya saa sita na ushee hivi na baadaye wakongwe waakaanza kuangusha libeneke la bandika bandua,palikuwa hapatoshi uwanjani hapo.Pichani ndio kama uonavyo umati wa wakazi wa Dodoma ulivyoamua kujiramba kwa staili ya aina yake.

No comments: