AU Yawabana Viongozi Wasiotii Demokrasia

Alisema Afrika ni lazima ilinde misingi ya kidemokrasia, utawala wa sheria na haki za binadamu zinazoonekana sasa katika bara hilo kwa kuheshimu uchaguzi wa kidemokrasia na matokeo yake. Utamaduni wa nchi kufanya uchaguzi muda unapofika, alisema umeimarika na kutekelezwa na nchi kadhaa za Afrika, akisema tangu kuanzishwa kwa Bunge la Afrika mwaka 2004, uchaguzi wa kidemokrasia na wa wazi umefanywa katika nchi 45; mwaka pekee nchi tano zimefanya uchaguzi. Alisema wakati Afrika inafurahia maendeleo hayo ya kidemokrasia, bado kuna matukio machache yasiyofurahisha, na amelitaka Bunge la Afrika kuunga mkono juhudi za kulinda demokrasia, haki za binadamu na utawala wa sheria.
Rais Kikwete amesema analitarajia Bunge hilo kuwa chachu na nguvu ya kulinda misingi hiyo, kwa kujadili na kuwasukuma viongozi wa Afrika juu wa wajibu wao wa kuheshimu utawala bora, kulinda haki za binadamu na kuwajibika kuhakikisha utawala wa sheria katika nchi wanazoziongoza. Mapema akimkaribisha Rais Kikwete kufungua kikao hicho cha Bunge, Rais wa Bunge hilo, Balozi Getrude Mongela, alisema lina wabunge 245 kutoka nchi 47 zinazowakilishwa.
Habari Kwa Hisani Ya HabariLeo
Habari Kwa Hisani Ya HabariLeo
No comments:
Post a Comment