Tuesday, July 15, 2008

Obssession Wachengua
Zenji...
Usiku wa kuamkia jana saa nane wazanzibari na wapenzi wa muziki ndio waliondoka kwenda kulala baada ya Obssession kutoka Uganda kumaliza kushambulia jukwaa na mauno yao hatari na sauti bomba. hawa jamaa ni kiuno bila mfupa nini.

Muziki ulianza saa tatu baada ya kuona moja ya filamu zinazoonyesha utamaduni maana yake nini,filamu inayomhusu mzee nzawose.

Walahi ililipa kukaa muda wote,makamuzi yalikuwa ni babu kubwa.Ililipa kuwaona watanzania wakiselebuka ndani ya jukwaa akina Nakaaya,Mwasiti huku wakipigwa tafu na back up ya THT walahi haikuwa mbaya.Nilisema ni usiku hatari,kweli ilikuwa hatari.

Na kama masikhara mdogo wake Banana yule wakike maunda anaonekana kama mtu wa kuangaliwa siku za baadaye.Kama Kawaida Blog hii inatoa shavu kwa Mdau(Kaka)Msimbe Lukwangule kwa Updates hizi mwanana kabisa kutoka Zenji..

No comments: