Thursday, July 31, 2008

Kimwana wa Face Of Tanzani aelekea
Sauzi Afrika..



Pichani ni Mkurugenzi wa Beautiful TanzaniA Agency,Irene Kiwia,(kushoto),akiwa na kisura wa Tanzania (Face of Tanzania)Emmy Melau(katikati),muda mfupi kabla ya kuondoka Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere,Dar es Salaam leo.
---
Na Msimbe Lukwangule.
Mshindi wa kwanza wa shindano Face of Afrika,Emmy Melau ameondoka nchini leo kuelekea nchini Afrika kusini ambako amekwenda kufanya kazi katikakampuni ya O Model Africa aliyojiunga nayo kwa mkataba wa mwaka mmoja.

Emmy alipata tiketi ya kuwa kisura wa Tanzania katika shindanolililofanyika hivi karibuni, alifanikiwa kutwaa ushindi huo baada yakuwabwaga wenzake katika hatua ya fainal iliyofanyika jijini Dar esSalaam.Akizungumza katika Uwanja wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar esSalaam kabla ya kuondoka,Emmy alisema anawashukuru watanzania kwakumuunga mkono wakati wa shindano la kumsaka kisura wa Tanzania nakuwapongeza waandaaji wake kampuni ya Beautiful Tanzania Agency.

Emmy alisindikizwa na baadhi ya ndugu zake,akiwemo mama yakemzazi,Oliver Thomas, mama yake mlezi,Nancy Wilson,na dada yake HappyLaizer,pamoja na mkurugenzi wa Beautiful Tanzania Agency,Irene Kiwiaaliyekuwa amefuatana na Flora Lauro.Emmy aliahidi kufanya kazi kwa bidii zote ili kuliletea sifa taifa la Tanzania kutokana na utendaji wake.

1 comment:

Anonymous said...

am happy that god can do his wonders the twins who were born in geramny one black and one white they are reminding us that god loves us regarless. This should be a great teaching to all beings how can you claim you are one thing.