Friday, July 25, 2008

Blanchard De Plaizir kukamua na Lady
Jaydee na Wana wa
Akudo Sound....
Blanchard De Plaizir katika pozi.
------
Mwanamuziki anayekuja kwa kasi toka Jamhuri ya Congo Blanchard Deplaizir amesema kuwa yuko katika maandalizi ya kwenda Dar Es Salaam kwa ajili ya kurekodi nyimbo tatu ambazo amesema atafanya kolabo na wanamuziki wa Kitanzania.Blanchard ambaye anapiga muziki wenye mahadhi ya Rhunba,na hata Rap pia maskani yake yako jijini London baada ya kuhamia huko yapata miaka 20 iliyopita na shughuli zake za kimuziki anaziendeleza huko.

De Plaizir akiwa na kikosi chake mbele ya mashabiki lukuki nakati ya Londone.
Akiwa Tanzania Blanchard atafanya kolabo na Ali Kiba,Lady Jay Dee na Akudo ili kuweka vionjo vya muziki wa Africa Mashariki hasa Tanzania ambao anasema kwa kiasi kikubwa anauhusudu sana.

Akiongea na Spoti na Starehe jioni hii Blanchard alisema,“nimeongea na Meneja wa Lady Jay Dee Gadna Gee Habash, kimsingi wamekubaliana na terms na nia yangu nafikiri safari itakuwa mwezi wa nane au hadi wa tisa”

“Nimesikia nyimbo za Akudo nimewapenda sana wanaimba vizuri nafikiri safari yangu itakuwa na mafanikio huko”aliongeza Deplaizir.

Aidha kwa sasa Blanchard anasema anafanya kazi na Bongo Dj,timu ya madj watanzania walioko nchini Uingereza ambao ni mabingwa wa matamasha kwa wanamuziki toka Afrika hasa Tanzania,katika mwezi ujao Blanchard atafanya maonyesho mawili yaliyoandaliwa na Bongo Family/DJ tarehe 22 atakuwa reading na tarehe 23 watafanya Milton Keynes,hii yote ni live band akishirikiana na akina dada mastage shoo wake.

Katika Albamu yake ya sasa Blanchard alishirikisha watu mbalimbali akiwemo Titina Alcapone ambaye alipata kuwa mwanamziki wa Wenge BCBG kwa muda mrefu kabla ya kwenda kwa Koffi Olomide na kisha kutoka kivyake.Habari na Mdau Pius Pius.

No comments: