Wednesday, July 30, 2008

Balozi wa Tanzania nchini Uingereza
azindua Kitabu cha Kiswahili cha
“Mbinu za Ujasiriamali” ...
Dr Imani (Kulia)akimkabidhi nakala ya Kitabu cha Ujasiriamali Mh. Mwanaidi Majaar – balozi wa Tanzania London na maafisa wengine wa ubalozi.
Dr Imani akimkabidhi nakala ya kitabu Mh. Bi Suzan Stephen–
Mzee katibu wa CCM London (UK).
----
Kitabu hiki kinaeleza maana na umuhimu wa kupata mafunzo ya ‘Ujasiriamali’.Kinaeleza kuwa ili uwe mjasiriamali mwenye mafanikio huna budi kufahamu mambo
mbalimbali kama vile:

. Mbinu za kukabili ongezeko la ushindani wa kibiashara
.Jinsi ya kuunganisha mtaji na uzoefu wako ili kupata mafanikio zaidi
.Nafasi na umuhimu wa matumizi ya teknolojia na utunzaji kumbukumbu na taarifa sahihi za kibiashara
.Nafasi na umuhimu wa utafiti wa kibiashara kabla na wakati wa kuendesha biashara ili kuongeza ubunifu mpya katika biashara yako.

Kwa hiyo,hiki ni kitabu kidogo kinachotoa mwongozo juu ya mbinu za kuwa mjasiriamali makini na mwenye mtazamo wa kimaendeleo.Kimeandikwa kwa lugha nyepesi na ambayo inaeleweka kwa urahisi.

Dkt Imani Silver Kyaruzi,ni mwalimu na mtafiti wa ujasiriamali na uchumi.
Ana Shahada ya Udaktari wa Falsafa(PhD)ya Uchumi na Ujasiriamali(Chuo Kikuu cha Birmingham)

Shahada ya Pili(MBA)katika Ujasiriamali na Biashara(Chuo Kikuu cha Central England)
na Shahada ya Kwanza (BA Hons) katika Biashara na Utawala kutoka Chuo Kikuu cha Woverhampton.
Wachapaji:
Mkuki na Nyota Publishers
www.mkukinanyota.com
Kwa nakala wasiliana na
Ndugu Deo Simba:

No comments: