Thursday, July 31, 2008

Toleo la Raia Mwema Wiki Hii...
*Giza nene kifo cha Wangwe



TANGU baada ya habari za kifo kwa ajali ya gari za Mbunge wa Tarime Chacha Zakayo Wangwe (52)zilipofahamika hapa juzi usiku,mji huu ulikumbwa na simanzi kubwa.

Hiyo ilitokana na sababu kwamba wengi wa watu hapa,hata umma wa kawaida,ulimwona Wangwe kuwa mmoja ya wapambanaji wazuri ndani ya kundi dogo la Wabunge wa Upinzani wapatao 43 sasa.
Wangwe alifariki dunia katika eneo la Pandambili,Kongwa,majira ya saa 2.55 usiku akitoka hapa kwenda Dar es Salaam ambako taarifa zinasema alikuwa awahi mazishi ya mwana Tarime mwingine,Bhoke Mnanka,ambaye anatarajiwa kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni.kwa mengi zaidi juu ya Habari hii na Makala Mbalimbali zilizokwenda shule ikiwemo Rai ya Jenerali Ulimwengu Bofya na Endelea ......>>>>>

No comments: