Thursday, December 17, 2009

Dr Lawrence Gama Afariki Dunia
MBUNGE wa zamani wa Songea Vijijini Dk Lawrence Gama(Pichani),amefariki dunia jana mchana katika hospitali ya Agha Khan baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kansa ya mapafu.Katibu wa Itikadi na Uenezi ya CCM,John Chiligati, alithibitisha kutokea kwa kifo hicho na kuongeza kuwa taarifa zaidi ya kifo hicho zitatolewa leo.
Alisema CCM imepokea kwa mshtuko taarifa za kifo hicho kwa kuwa kiongozi huyo alikuwa ni mmoja wa wazee waliotumikia Tanzania kwa uadilifu na mfano wa kuigwa na vijana.“CCM tumempoteza mtu muhimu ambaye alijitolea kwa muda mrefu kutumikia nchi yake kwa kuwa alishika nyadhifa mbalimbali muhimu hali ambayo vijana wa sasa wanapaswa kuiiga,” alisema Chiligati.

Alisema Gama katika uhai wake pamoja na kuwa mbunge ni mmoja wa waanzilishi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi(JWTZ),aliwahi kuwa Katibu wa CCM na pia aliwahi kuwa mkuu wa Usalama wa taifa nchini.

No comments: