Thursday, March 12, 2009

mzee ruksa aliposhambuliwa jukwaani juzi
rais mstaafu alhaj ali hassan mwinyi akihutubia baraza la maulidi ukumbi wa diamond jubilee hall juzi. kulia kwake ni mzee rashidi mfaume kawawa
alhaji mwinyi akiendelea na hotuba yake
alhaj mwinyi akifafanua jambo
alhaj mwinyi mara baada ya kushambuliwa jukwaani
kama kawaida yake alhaj mwinyi tabasamu halikumtoka pamoja na maswahiba yaliyomsibu
alhaj mwinyi akiondoka ukumbuni huku tabasamu lake likiwaka usoni pake
alhaj mwinyi akiagwa na walohudhuria baraza la maulidi
mara baada ya kumshambulia alhaj mwinyi kijana aliyefanya kituko hicho akigombewa kama mpira wa kona na wadau wenye hasira
maafisa usalama walifanya kazi ya ziada kumuokoa mshambuliaji huyo

ilikuwa patashika na nguo kuchanika. wanausalama walijitolea maisha yao kumuokoa kijana huyu
karibu kila aiyekuwepo alitaka kumuadhibu mshambuliaji huyo
wanausalama walifanya kazi yao kikamilifu kuokoa maisha ya mshambuliaji huyo
haikuwa kazi ndogo kumuokoa
mbinu zote zilitumika kuhakikisha mshambuliaji huyu hapatwi na sheria mkononi
kazi ilikuwa nzito kumuokoa
dakika nne za vurugu hilo zilionekana kama masaa mia nne
hatimaye mshambuliaji aliwekwa kwenye gari na kukimbizwa kituo cha polisi...
Habari ni kwamba mtuhumiwa Ibrahim Said Sultan maarufu kama (Ustaadh) aliyemshambulia Rais Mstaafu Ally Hassan Mwinyi kwa kumpiga kofi wakati akitoa hotuba katika Baraza la Maulid katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar juzi atafikishwa mahakamani leo kujibu shtaka la kushambulia hadharani.
Kamanda wa mkoa maalumu wa kipolisi wa dar afande Selemani Kova amesema upelelezi wa tukio hilo unaendelea ikiwa ni pamoja na kupima afya na akili yake pia kujua kama mtuhumiwa ni mwanaharakati na kama alikula njama na watu wengine kufanya kitendo hicho.
Kamanda Kova ameongeza juwa mtuhumiwa amehojiwa na kueleza kuwa hakuwa na nia ya kumdhuru Rais Mstaafu huyo lakini kwa kuwa ni mtu maarufu na anapendwa na watu wengi aliona akimfanyia kituko hicho atakuwa amefikisha ujumbe wake ambapo kijana huyo anapinga waislamu na wakristo kushirikiana katika kusherehekea sikukuu zao.
Kijana huyo amesema pia kuwa hapendi viongozi wa dini kushawishi jamii kutumia kondom kwani kwa mujibu maelezo yake hiyo ni kahamasisha matendo maovu ya zinaa ambayo hayakubaliki kidini.
















No comments: