Wednesday, May 13, 2009

hospitali ya amana yapata maabara ya kisasa
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii David Mwakyusa akikata utepe kuashiria uzinduzi maalumu wa maabara ya kisasa iliyojengwa na Abbott Fund kwa msaada wa wananchi wa Marekani,(kulia)Makamu wa Rais wa Abbott Fund Chrity Wistar,(kushoto) Mganga Mkuu wa Hospital ya Amana Willy Sangu.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana Dk. Willy Sangu akimpokea Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii David Mwakyusa,kuja kuzindua rasmi maabara ya kisasa iliyojengwa na Abbott Fund kwa msaada wa wananchi wa Marekani.


Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii David Mwakyusa (kushoto)akisaini kitabu cha wageni wakati wa uzinduzi wa maabara ya kisasa Amana Hospital iliyojengwa na Mfuko wa Abbott Fund,(katikati) Makamu wa Rais wa Abbott Fund Christy Wistar,(kulia) Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ilala Prof Dafrosa Limo.

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii David Mwakyusa,akizungumzia jambo ndani ya maabara ya kisasa mara baada ya kuzindua rasmi Amana Hospital iliyojengwa na Mfuko wa Abbott Fund kwa msaada wa wananchi wa Marekani,Kulia kwake ni Meneja wa maabara Costantine Mzava,Kushoto kwake ni Mganga Mkuu wa Hospital ya Amana Willy Sangu.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii David Mwakyusa,(kulia)Akipatiwa maelezo na Makamu wa Rais wa Abbott Fund Christy Wistar juu ya namna ya vifaa vya maabara ya kisasa vitakavyotumika mara baada ya kuizindua rasmi,(katikati) Meneja wa maabara Costantine Mzava,Kushoto kwake ni Mbunge wa Ilala Musa Azani Zungu,Maabara hiyo ilijengwa na Abbott Fund kwa msaada wa watu wa Marekani





No comments: