Thursday, March 18, 2010

TembeaTz.blogspot.com ndio unapata mambo haya. picha za wa chini (Duma)

Duma anajulikana kwa jina la wa chini kwa kuwa yeye ni mzee wa mbio mbio. Hana ujanja wa kupanda miti kama binamu yake, wa juu (chui). Tofauti kati ya wa chini (duma/Cheetah) na wa juu (chui/leopard) ni kwamba wa juu ana umbo lililojengeka kinamna wakati wa chini yeye ni lightweight - kimbaumbau. Hali hii ndio inayomfanya awe na uwezo wa kutimua mbio na kuwazidi wapinzani wake.

Wa chini hupendelea kukaa maeneo ya wazi (open grass lands) maeneo ambayo yanampa nafasi ya kuchanganya spidi na kuweza kuwashinda wapinzani wake. Hapa nyumbani, hawa jamaa wanashamiri sana Serengeti NP kwa kuwa ukanda wa nyasi wa huko unawapa advantage ya kuweza kukimbia kwa spidi ya juu. Pia wanapatikana Ngorongoro crater.

Anapokuwa anakimbia, wa chini hutumia mkia wake kuweza kupata balance akiwa ktk spidi kali. Hii ni muhimu kutokana na hali ya kwamba mwili wake ni mdogo (kimbaumbau). Mkia wake ni nyenzo muhimu sana kwake.
Wa juu hufanya issue zake mida ya mchana na usiku hupumzika (mara nyingi). Kutokana na yeye kuwa ni mnyama anaewinda mchana, pembezoni mwa macho yake kuna rangi nyeusi ambayo kazi yake ni kuweza kumsaidia kuona vizuri akiwa kwenye jua kali. Rangi hii huwa kama sun glasses kwake. Hii ni hali ambayo wanyama wengi wanaofanya shughuli zao mida ya mchana huwa nayo ktk macho yao.

Picha hizi zilipigwa na wadau waliotembelea Ngorongoro Crater hivi karibuni na kuwafuma hawa wajuu wakiendelea na inshu zao.

No comments: