Monday, March 22, 2010

naomba nijuzwe katika hili
kama kawaida jana jumapili nilikuwa na washikaji tukiwa tunatazama tv. Katika channel moja hivi hapa jijini na pia ni maarufu na ilikuwa kama mida ya saa mbili hivi usiku tukiwa tunataka kujua yaliojiri kwa siku hiyo.
Kweli muda ukafika tukaanza kuangalia habari tukakutana na kisa hiki au kilichonifanya nikose jibu nakuja huku jamvini kwangu japo kupata mawili matatu kutoka kwenu.
Nayo ni uvaaji wa sare za chama katika mikutano isiyo ya kichama nikimaanisha mikutano ya kiserikali hii inakuwaje naombeni mnijuze.

1 comment:

Anonymous said...

Ni ujinga tu wa viongozi na wanachama wa ccm, hawajatambua bado tuko kwenye karne ipi, ni ajabu leo kiongozi wa serikali anataja itifaki katiko hotuba kwa ku-refer "viongozi wa chama na serikali" katika sikukuu ya mei mosi wakati viko vyama kibao vya siasa na vyama vya wafanyakazi