Simba wadungwa Jezi
Mpya..

---
Pazia la Ligi Kuu soka Tanzania Bara linafunguliwa leo kwa kuchezwa mechi mbili katika viwanja viwili tofauti.Ligi hiyo ambayo ni mara ya pili inafanyika kwa mfumo mpya wa kufuata kalenda ya Shirikisho la Soka la Kimataifa FIFA,itashirikisha timu 12.Katika Uwanja wa Taifa,timu ngeni iliyopanda msimu huu ya Villa Squard itakuwa mwenyeji wa wakongwe Simba.
Simba ilimaliza ligi ya mwaka jana ikiwa nafasi ya tatu kwa kujikusanyia pointi 42 nyuma ya mabingwa wa ligi hiyo,Yanga kwa pointi saba na nyuma ya Prisons iliyoshika nafasi ya pili kwa pointi tatu.Habari hii na Anastazia Anyimike,Picha na Mrocky
No comments:
Post a Comment