Friday, November 28, 2008

siku za mwizi zikifika,hazikwepeki.!


"Jamani mwenzenu najuta kwa kipigo,sijui kama ntarudiao ai"! Mtuhumiwa akisikilizia maumivu baada ya kupata kifinyo kutoka kwa watu wenye hasira kali


Hapa mtuhumiwa akionesha baadhi ya vitasa alivyokutwa navyo



"Twende fanya haraka alaa"!
Mtuhumiwa akiburuzwa kupelekwa kituo cha polisi kati baada ya kupata kibano
Mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la William Matiku au William Ngabo a.k.a Baba Nyandalo amejikuta akipata kipigo cha nguvu kutoka kwa wakazi/wafanyakazi wa jengo la kitega uchumi a.k.a NIC leo mchana baada ya kutuhimwa kuiba vitasa vya milango ya jengo hilo lenye vikwangua anga 14.Mzee huyo ambaye alieleza kuwa ni mkazi wa Majumba sita -Ukonga aliokolewa na wasamaria wema na kumpeleka kituo cha polisi central.Aidha baadhi ya watu waliokuwepo kwenye tukio hilo walieleza kuwa hiyo ndio tabia yake sugu aliyonayo ya kukwapua vitu vya watu

No comments: