miriam odemba apongezwa jana usiku
Mkurugenzi wa Kampuni ya Campass Communication Maria Sarungi akizungumza mbele ya wageni waalikwa kwenye hafla fupi ya kumpongeza mlimbwende wa Dunia namba 2 Miriam Odemba baada ya kuibuka mshindi wa pili katika mashindano ya miss Earth yaliyofanyika hivi karibuni nchini Ufilipino. Hafla hii imefanyika jana usiku ndani ya hoteli ya New Africa.Maria Sarungi alisema kuwa Odemba bado ana kazi kubwa inamkabiri mbele yake kuhakikisha taji hilo linabaki kwa Tanzania, kama vile haitoshi ameongeza kuwa Odemba pia atashiriki kufanya kazi mbali mbali za kijamii hapa nyumbani na pia desemba 28 atarejea nchini Filpine kuungana na mshindi wa kwanza katika kufanya kazi za kijamii nchini humo.Pia atatembelea nchi mbalimbali ikiwepo Singapore na nyinginezo.Aidha Maria amebainisha kuwa Miriam amepata mkataba wa mwaka mmoja wa kufanya kazi nchini humo
No comments:
Post a Comment