Tuesday, November 25, 2008

mdau yuko njia panda tumsaidie.!

Niko njia panda sana kipindi hiki.
ILA NINGEOMBA USITOE JINA AU UTAMBULISHO WANGU KWA HILI.
ASANTE KWA KUTUWAKILISHA MTANDAONI.


Wana jukwaa,ningeomba ushauri wenu.Nimekua na mpenzi wangu kwa zaidi ya miaka miwili ingawa alikua anaishi kwao lkn alikua akija kwangu na hata kushinda au kulala siku zingine.Sasa hivi majuzi mdogo wangu wa kiume alihamia kwangu baada ya chuo chao kufungwa ghafla na hivyo tukawa tukiishi nae.

Tatizo likaanzia hapo siku moja nikarudi nkampa mdogo wangu hela akanunue vitu kwa ajili ya kupika na mpenzi wangu huyu akaanza kulalamika sana mpaka sasa bado hatujapata mwafaka.Zaidi anadai kua kuja kwake kwangu atasitisha kwani inaonekana amekua akikwaza ndugu zangu,na pia anadai kua huyu mdogo wangu hamrespect na pia anaona kama yeye anamzibia uhuru wa kukaa nami kama ndugu yake.

Nilipokaa na mdogo wangu kumwuliza yeye alikana kabisa/katu katu kwamba hana tatizo nae na pia anamheshim sana kama shemeji yake,kumweleza huyu mpenzi wangu akaruka akasema ni mnafiki na wala hamaanishi hivyo,cha ajabu nimemwambia niwakutanishe yeye na mdogo wangu amekataa akisema hawezi kukaa na kubishana shemeji yake yeye atakachokifanya ni kutokuja kwangu.

JE HAPO MIMI NIFANYEJE KWANI NIKO NJIA PANDA,nafikiria niachane nae au la kwani simwelewi ananimaanishia nini.jana nikawa nimempa hatima kua kama hawezi kuishi na ndugu zangu kwa upendo kama anaonipa mimi basi sioni sababu ya kuwa nae akanitumia msg kua NITAFUTE ATAKAE WEZA WAPENDA NDG ZANGU.

Nimekua njia panda kwani kiukweli nlikua na malengo makubwa nae coz NILIMPENDA ila naona nashindwa.Je nifanyeje?
Mdau alie njia panda!!

No comments: