Saturday, November 29, 2008

kumuona fat joe buku kumi na kumi na tano.!


Ebwanaee ngoma imeiva sasa.! Mwanamuziki wa hip hop kotoka Unyamwezini Fat Joe na mwanadafada mwingine machachari sana katika anga za kufoka foka aitwaye Eve E na mwingine wa tatu (jina tega sikio na macho hapa hapa jamvini) wanatua jijini Dar desemba 8 na kuangusha bonge la shoo katika viwanja vya Gymkana ambapo kiingilio kimepangwa kuwa ni kati ya 10,000/= (mapema) na 15,000/=(getini) kwa kila kichwa.
Aidha katika shoo hiyo itakayokuwa ya aina yake na isio na ubaguzi kabisa kwa wasanii wake wa nyumbani,katika kuipamba shoo hiyo atakuwepo mtu mzima Pro Jay,Mangwea,Mr Blue pamoja na Mwana-FA na Ambwene Yesaya a.ka. AY watakaozindua albamu yao kwa pamoja itakayoitwa Habari ndiyo hiyo na wasanii wengine kadha wa kadha.
Wadau goma hilo lishawekwa wazi kila kitu, hivyo si ya kukosa kabisa, achana na suala la kuhadithiwa. ooh alifanya hivi,ooh alikuja na sijuiii niniiii aah haya maswali kama mtoto wa kijanja hupaswi kuuliza kiivyo,muhimu jichange mapema halafu Inawezekana au sio.Pamoja Wanajamvini

No comments: