Monday, November 24, 2008

ifm hali bado tete,hakuna muafaka.!


Hakuna aliyethubutu kuingia darasani,walithubutu


Mkuu wa chuo cha IFM Prof Joshua Dolie akizungumza hivi punde na wanafunzi

Kwa habari zilizopatikana hivi punde uongozi wa chuo cha IFM umetoa tamko kuwa Wanafunzi wanaotaka kufanya mitihani waingie darasani na wale ambao hawataki kufanya mitihani watawanyike/waondoke eneo la chuo, wale ambao wako hosteli na hawataki kufanya mitihani wabebe vitu vyao waondoke chuoni hapo.

Lakini wanafunzi hao kwa kuonesha umoja wao wakaanza kumzomea mkuu wa chuo mpaka anaondoka eneo hilo ambalo wanafunzi walikuwa wamekusanyika na hakuna muafaka uliokuwa umepatikana.Kuhusu uongozi wa chuo upande wa wanafunzi wao wametoa tamko la kutoingia madarasani kufanya mitihani mpaka uongozi wa chuo utakapo rekebisha ratiba hiyo ambayo inaonekana kuwachanganya wanafunzi hao.

Wanafunzi hao wakakubaliana kuwa wakae chuoni hapo mpaka majira ya saa kumi ili kuwadhibiti wale watakaoonekana wanasaliti wanafunzi wenzao kwa kuingia madarasani na kufanya mitihani.Uongozi huo wa wanafunzi umewataka wanafunzi wenzao kushinikiza uongozi wa chuo kubadili ratiba hiyo ya mitihani kwa kuendelea na mgomo hapo kesho.

Mpaka kamera ya INAWEZEKAN inatoa eneo la tukio hakuna muafaka uliopatikana baina ya wanafunzi na uongozi wa chuo

No comments: