Saturday, November 29, 2008

mramba na yona kuendelea kusota rumande



Wh. Basil Mramba na Daniel Yona wataendelea kusota tena rumande hadi Jumatatu pamoja na mahakama kuu kuwalegezea masharti ya dhamana.Mahakama kuu katika uamuzi wake wa leo, ililegeza sharti la kuwataka washitakiwa hao kutoa fedha taslimu, badala yake ikawapa mbadala wa kuwasilisha hati za mali yenye thamani ya Sh bilioni 2.9 kila mmoja.


Uamuzi wa kuwataka washitakiwa waweke fedha taslimu ulitolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na Hakimu Hezron Mwankenja. Lakini sharti hilo lililegezwa jana na mahakama hiyo ya juu.Uamuzi huo wa Jaji Njegafibile Mwaikugile licha ya kupokewa kwa furaha na ndugu wa washitakiwa, haukuwasaidia sana kutokana na hati walizokuwa nazo kuonekana kuwa na dosari kadhaa ambazo zilihitaji uthibitisho kutoka kwa mamlaka zingine.

No comments: