Simba wadungwa Jezi  
 Mpya..
  
 Mwenyekiti wa Klabu ya Mpira wa Miguu ya Simba,Hassan Dalali  akiangalia kwa umakini jezi walizokabidhiwa na wadhamini wa Ligi kuu ya Soka  Tanzania Bara,Vodacom jana kwa ajili ya msimu mpya wa ligi unaoanza leo.Timu  zote zilikabidhiwa vifaa na wadhamini hao jana.---
 Pazia la Ligi Kuu soka Tanzania Bara linafunguliwa leo kwa  kuchezwa mechi mbili katika viwanja viwili tofauti.Ligi hiyo ambayo ni mara ya  pili inafanyika kwa mfumo mpya wa kufuata kalenda ya Shirikisho la Soka la  Kimataifa FIFA,itashirikisha timu 12.Katika Uwanja wa Taifa,timu ngeni  iliyopanda msimu huu ya Villa Squard itakuwa mwenyeji wa wakongwe Simba. 
  Simba ilimaliza ligi ya mwaka jana ikiwa nafasi ya tatu kwa  kujikusanyia pointi 42 nyuma ya mabingwa wa ligi hiyo,Yanga kwa pointi saba na  nyuma ya Prisons iliyoshika nafasi ya pili kwa pointi tatu.Habari hii na Anastazia Anyimike,Picha na Mrocky
 
No comments:
Post a Comment