Wednesday, August 27, 2008

Adha na karaha za barabarani

Hapa baada ya mshike wa hapa na pale ndio akatokea trafiki kama unavyomuona pichani,akielekea kwenye ajari husika kuweka maambo sawa



Wajameni njiani kuna adha na karaha nyingi sana za kukatisha tamaa kama kutakosekana umakini na ustaarabu hasa kwa hawa madereva wetu!,nayasema haya kwani yametokea mwishoni mwa wiki wakati Mdau mmoja wa blog hii alipokuwa anakwenda zake Moshi, njiani maeneo ya msata hivi akakutana na bonge la foleni kama hivi pichani, akajihisi kama vile yuko Dar,asubuhi flani hivi anawahi kazini, akawa anajiuliza hali hii inakuwa vipi na huku!,kumbe bwana Lori limeanguka na kuziba barabara, ilikuwa yapata kama saa tano na ushehe hivi asubuhi, ebwenae shughuli ilikuwa pevu.Lakini kwa bahati nzuri alitokea trafiki fasta na kuirekebisha ile hali na magari yakaanza kutambaa kama kawa.

No comments: