Monday, August 25, 2008

kumbukumbu ya miaka 3 ya vivian David Tilya



Mpendwa wetu Vivian David Tillya tarehe 21/08/2008 umetimiza miaka 3 tangu ulipotutoka ghafla bila ya neno la kwa heri katika ajali ya gari mbaya ya barabarani iliyotokea Mbwewe,Jumapili asubuhi tarehe 21.08.2005 ukiwa njiani kwenda Arusha kuungana na familia katika jubilee ya ndoa ya wazazi wako.

Jiachie na kwa niaba ya wafanyakazi wenzako wa Clouds Fm 88.4,Prime Time Promotions Ltd ikiwemo familia yako,ndugu jamaa na marafiki zako tunakukumbuka daima kwa wema,ucheshi,huruma heshima,hekima na busara zako kwa watu wote wakubwa kwa wadogo.


Nafasi yako katika familia na jamii yote bado iko wazi na mioyoni mwetu umejaa tele.
Pumzika kwa amani dada yetu mpendwa Vivian-AMEN


No comments: