Friday, August 29, 2008

konda shujaa apongezwa

Pichani ni Kondakta wa Basi linalofanya safari zake jijini Dar es Salaam akiongoza magari baada ya foleni kubwa ya kwenye makutano ya barabara ya Lumumba na Uhuru.


Kujitolea kwa kondakta huyo kati ya Makondakta wote waliokuwapo hapo, ni moja ya kazi ya kila raia wa nchi kujitolea wakati jambo au mambo yoyote yanayojitokeza aidha kwa bahati mbaya, bila ya makusudio au kwa makusudio.


Kujitolea kusawazisha ya wenzako au kusawazisha kwenye kila jambo linaloelekea pabaya ni haki ya kila raia kumshauri raia mwenzako ili ndugu au jamii au kijiji au nchi isielekee pabaya.


Kwa nchi kama Uingereza wanaita "Duty of Care".


Je, huyu ni wewe?Kwa yeyote anayemjua kijana huyo (pichani) atume namba yake ya simu,



tuna zawadi ndogo tu ya kumpa ndugu yetu huyo mwenye mfano mzuri, ahsante.Na aliyepiga picha hii wa gazeti la This Day, tunampa ahsante.
Na Kaka Issa Michuzi (Happy Birthday on the 28th August 2008).
Zenjydar Community Association inawatakia Watanzania wote duniani, RAMADHAN KAREEM.
Mhariri,
Zenjydar Community Association


No comments: