konda shujaa apongezwa
 
Pichani ni Kondakta  wa Basi linalofanya safari zake jijini Dar es Salaam akiongoza magari baada ya  foleni kubwa ya kwenye makutano ya barabara ya Lumumba na  Uhuru.
Kujitolea kwa  kondakta huyo kati ya Makondakta wote waliokuwapo hapo, ni moja ya kazi ya kila  raia wa nchi kujitolea wakati jambo au mambo yoyote yanayojitokeza aidha kwa  bahati mbaya, bila ya makusudio au kwa makusudio.
Kujitolea kusawazisha  ya wenzako au kusawazisha kwenye kila jambo linaloelekea pabaya ni haki ya kila  raia kumshauri raia mwenzako ili ndugu au jamii au kijiji au nchi isielekee  pabaya. 
Kwa nchi kama  Uingereza wanaita "Duty of Care". 
Je, huyu ni wewe?Kwa  yeyote anayemjua kijana huyo (pichani) atume namba yake ya simu,  
tuna zawadi ndogo tu  ya kumpa ndugu yetu huyo mwenye mfano mzuri, ahsante.Na aliyepiga picha hii wa  gazeti la This Day, tunampa ahsante. 
 Na Kaka Issa Michuzi  (Happy Birthday on the 28th August 2008).
 Zenjydar Community  Association inawatakia Watanzania wote duniani, RAMADHAN  KAREEM.
 Mhariri,  
 Zenjydar Community  Association
 
No comments:
Post a Comment