Monday, August 25, 2008

fanya kweli ya tanzaniano yaingia sokoni



Wasanii wa muziki wa kizazi kipya wanaounda kundi la Tanzaniano,linalojumuisha wasanii 3 ambao ni Daz Baba,Ally Mbongo pamoja na Lalumba wameikamilisha albamu yao kwanza inayoitwa Fanya kweli.

Albamu hiyo yenye jumla ya nyimbo kumi, imerekodiwa katika studio tofautitofauti za hapa jijini ili kuinogesha albamu hiyo,akizunguma na Jiachie leo mchana kiongozi wa kundi hilo Daz Baba amesema kuwa albamu hiyo tayari imekwishaingia sokoni kwa ajili ya mauzo.
Daz amezitaja baadhi ya nyimbo zilizomo kwenye albamu hiyo kuwa ni Modo wa afrika,Demu ni demu,mambo mengi,hawajui,Fanya kweli na nyinginezo.Aidha amezitaja studio zilizoipika vema albamu hiyo kuwa ni Mj Records,Sound Crafters pamoja na Mo Records ya jijini Mwanza
Daz Baba na Lalumba ni baadhi ya wasanii walitikisa mno wakiwa ndani ya kundi lao la awali lililoitwa Daz Nundaz akiwemo na Ferooz,ambapo kwa sasa kundi hilo limebaki jina

No comments: