Rais Kikwete atembelea  Ofisi za
 USAID  na USTDA  Nchini  
 Marekani..
 
Rais Jakaya Kikwete akilakiwa na Mkuu wa kitengo cha elimu cha  shirika la misaada ya kimataifa la marekani USAID Dr.Sarah Moten alipotembelea  Ofisi hizo jana.katika mkutano wao Dr Moten alitangaza msaada mpya kusaidia  ununuzi wa vitabu vya sayansi kwa shule za sekondari nchini wenye thamani ya  dola milioni 1.5 za kimarekani,Rais Kikwete yupo nchini Marekani kwa mwalimo  Maalum wa Rais George Bush.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh.Bernard  Membe(Kulia)na Mkurugenzi wa wakala wa biashara na ushirikiano wa kimataifa wa  marekani(USTDA)Mama Leocadia zak wakitia saini mkataba wa makubaliano ambapo  wakala huo utaipatia Tanzania kiasi cha dola 600,000 za kimarekani kuisaidia  sekta za umeme,mafuta na gesi nchini Tanzania.Rais Kikwete yupo nchini Marekani  kwa Mwaliko Maalum wa Rais George Bush.Picha na Freddy Maro/Ikulu
No comments:
Post a Comment