
Hatua hizi za Kodi ya Mapato kwa pamoja zinatarajiwa kuongeza mapato ya Serikali kwa kiasi cha shilingi 4,353 milioni.
C. Sheria ya Ushuru wa Bidhaa:-
1. Mheshimiwa Spika, inapendekezwa kufanya marekebisho katika Sheria ya Ushuru wa Bidhaa, Sura ya 147 kama ifuatavyo:-
(i) Kupunguza kiwango cha Ushuru wa Bidhaa kwenye mafuta mazito ya HFO kutoka Shilingi 117 kwa lita hadi Shilingi 97 ili kupunguza gharama ya uzalishaji viwandani, na kuongeza uwezo wa ushindani wa bidhaa zetu katika soko;
(ii) Kurekebisha mfumo wa kutoza Ushuru wa Bidhaa kwenye magari kutoka mfumo wa sasa wa kutoza ushuru wa asilimia 10 kwa magari yenye ukubwa wa ingini unaozidi cc2000 na kuwa na viwango viwili vya asilimia 5 na asilimia 10 kama ifuatavyo:
(a) Magari yenye ujazo wa ingini usiozidi cc1000 hayatalipa ushuru wa bidhaa;
(b) Magari yenye ujazo wa injini unoazidi cc1000 lakini hauzidi cc2000 kiwango cha ushuru kitakuwa asilimia 5 ya thamani ya gari;
(c) Magari yenye ujazo wa ingini unaozidi cc2000 kiwango cha ushuru kitakuwa asilimia 10 ya thamani ya gari.
(iii) Kurekebisha kiwango cha ushuru wa bidhaa katika huduma za simu za mkononi kutoka asilimia 7 ya gharama ya matumizi ya huduma, hadi asilimia 10 ya gharama hiyo. Sababu kubwa ya rekebisho hili ni kwenda sanjari na mfumuko wa bei (adjustment for inflation);
(iv) Kurekebisha kwa asilimia 12 viwango vya ushuru wa bidhaa kwenye bidhaa zinazotozwa ushuru huu kwa viwango maalum (specific rates), isipokuwa zile za mafuta ya petroli. Viwango vya sasa na vile vinavyopendekezwa ni kama ifuatavyo:
(a) Vinywaji baridi kutoka shilingi 48 kwa lita hadi shilingi 54 kwa lita;
(b) Bia inayotengenezwa na nafaka ya hapa nchini na ambayo haijaoteshwa, kutoka shilingi 173 kwa lita hadi shilingi 194 kwa lita;
(c) Bia nyingine zote, kutoka shilingi 294 kwa lita hadi shilingi 329 kwa lita;
(d) Mvinyo uliotengenezwa kwa zabibu inayozalishwa nje ya nchi kwa kiwango kinachozidi asilimia 25, kutoka shilingi 940 kwa lita hadi shilingi 1,053 kwa lita; na
(e) Vinywaji vikali, kutoka shilingi 1,394 kwa lita hadi shilingi 1,561 kwa lita.
(v) Kurekebisha viwango vya ushuru wa bidhaa kwenye sigara kama ifuatavyo:-
(a) Sigara zisizo na kichungi na zinazotengenezwa kutokana na tumbaku inayozalishwa hapa nchini kwa kiwango cha angalau asilimia 75, kutoka shilingi 4,775 hadi shilingi 5,348 kwa sigara elfu moja;
(b) Sigara zenye kichungi na zinazotengenezwa kutokana na tumbaku inayozalishwa hapa nchini kwa kiwango cha angalau asilimia 75, kutoka shilingi 11,266 hadi shilingi 12,618 kwa sigara elfu moja;
(c) Sigara nyingine zenye sifa tofauti na (a) na (b) kutoka shilingi 20,460 hadi shilingi 22,915 kwa sigara elfu moja;
(d) Tumbaku ambayo iko tayari kutengeneza sigara (“cut filler’) kutoka Shilingi 10,333 hadi shilingi 11,573 kwa kilo; na
(e) Ushuru wa “Cigar” unabaki asilimia 30.
D. Sheria zinazosimamia Kodi za Magari
2. Mheshimiwa Spika, inapendekezwa kufanya marekebisho yafuatayo katika kodi za magari:-
(i) Kupunguza viwango vya ada ya mwaka ya leseni za magari kama ifuatavyo:-
(a) Kwa magari yenye ujazo wa ingini usiozidi cc500 kutoka shilingi 50,000 hadi shilingi 30,000;
(b) Kwa magari yenye ujazo wa injini unaozidi cc500 lakini hauzidi cc1500 kutoka shilingi 80,000 hadi shilingi 50,000;
(c) Kwa magari yenye ujazo wa injini unaozidi cc1500 lakini hauzidi cc2500 kutoka shilingi 150,000 hadi shilingi 120,000;
(d) Kwa magari yenye ujazo wa injini unaozidi cc2500 lakini hauzidi cc5000 kutoka shilingi 330,000 hadi shilingi 140,000; na
(e) Kwa magari yenye ujazo wa ingini unaozidi cc5000 kutoka shilingi 175,000 hadi shilingi 150,000.
(ii) Kusamehe ada ya mwaka ya leseni za magari kwa matrekta ya kilimo
(iii) Kuongeza viwango vya ada ya usajili wa magari kutoka shilingi 27,000 kwa pikipiki na shilingi 90,000 kwa gari, hadi shilingi 35,000 kwa pikipiki na shilingi 120,000 kwa gari. Ada hii inalipwa mara moja tu na mwenye gari.
2 comments:
Concentrate to the things that could give information to the people.
This is a nice blog. I like it!
Post a Comment