Monday, August 11, 2008

Meseji za Mallya kwa Kabwe zanaswa,
Ajitambulisha ni mtaalam wa kompyuta,
Aomba tenda ya kuchapisha nyaraka,
Siri ya kukutana na Wangwe yabainika

*Ajitambulisha ni mtaalam wa kompyuta
*Aomba tenda ya kuchapisha nyaraka
*Siri ya kukutana na Wangwe yabainika
Na Hassan Abbas.

MBINU ya Bw. Deus Mallya (pichani),kijana aliyenusurika katika ajali iliyomuua mbunge wa Tarime, Bw. Chacha Wangwe,ambaye sasa anahusishwa na ujasusi,kuwaingia wanasiawa mashuhuri nchini na kujenga urafiki nao imebainika.

Mbinu hiyo imefahamika kufuatia uchunguzi wa gazeti hili kuzinasa meseji zake kadhaa alizowahi kumtumia Mbunge wa Kigoma Kaskazini(CHADEMA),Bw. Zitto Kabwe, ikiwa ni kabla ya kufahamiana na marehemu Wangwe.

Imebainika Mallya akijitambulisha kuwa ni mtaalamu wa mifumo mbalimbali ya programu za kompyuta katika uchapishaji wa nyaraka na vitu mbalimbali kabla ya kufahamiana na marehemu Wangwe,alijipenyeza kupitia kwa Bw.Kabwe akijinasibu kuwa angeweza kuifanya biashara hiyo vyema.

No comments: