Thursday, August 19, 2010

mtoto andrea anaomba msaada wa gharama za matibabu
Andrea akiwa kitandani pake

Mtoto Andrea Kipangula ni mtoto yatima kati ya watoto wanaosaidiwa vifaa vya shule na TAWLAE kwa msaada wa USAID/AED/ AGSP.

Ana miaka 10 (kumi) na anasoma darasa la nne (4) katika shule ya Kibao, wilaya ya Mufindi, kwa sasa, kwa masaa anayoweza kumudu anasoma shule ya msingi ya Makuburi, wilaya ya Kinondoni.

Mtoto huyu ana tatizo la kutopata choo kwa muda mrefu kwa vile njia yake ya haja kubwa inahitilafu. Madaktari wamemfanyia upasuaji mara saba hosipitali ya rufaa ya Muhimbili ili kurekebisha hali yake.
Kwa sasa imebidi atumie utumbo mkubwa kutolea choo ambao upo nje ya tumbo lake, hali ni ngumu kwa mtoto huyu.

Bibi yake ambaye ni mzee sana pamoja na shangazi yake ambaye ni mjane, hawana uwezo wa kumudu gharama za matibabu na maisha.
Wale watakaopenda kusaidia kwa njia ya benki,

tafadhali weka katika akaunti namba
0121030000838
ya NBC Samora Branch Dar-es-salaam,
ukishaweka tuarifu kupitia simu namba
0754-360215, 0754-360215, 0754-360215
au +255(22)2700085, +255(22)2700085, +255(22)2700085,
au fax pay in slip ya benki kwenye namba +255(22)2700090 +255(22)2700090 +255(22)2700090
Vinginevyo tuletee msaada kwenye ofisi zetu zilizopo
MARI-MIKOCHENI
Plot namba 24 “b”
Sam Nujoma Road
kuelekea kiwanda cha Cocacola,

Tafadhali tunaomba msaada wako ili kumsaidia mtoto Andrea.
Asante

No comments: