Friday, July 25, 2008

Tahadhari ya Mabomu Bangalore'
India..
---------------
Rais jumuiya ya wanafunzi wa Tanzania Bangalore India Bw Baraka Abdalla kange amewatahadharisha wanafunzi wote wa kitanzania kuwa kamini katika maeneo wanayoishi kutokana na mabomu yaliyolipuka leo mchana saa saba mchana na nusu mchana kwa saa za India.
Ndugu waTanzania wenzangu mabomu yametokea katika mji wetu wa Bangalore,nawaomba kila mmoja wetu kukaa nyumbani kwake na wale wachache mlioko hosteli mkae VYUMBANI KWENU,kutokana na hali mbaya ya mambomu iliyojitokeza leo katika maeneo ya MADIWALA, SAJAPURA ROAD, NAYANDAHALI, RAJA RAM MOHAN NEAR MALLYA HOSPITAL na ADIGUDI.
Nawaombeni waTanzania wote wa Bangalore kutulia majumbani katika siku hizi tatu bila kutembea maeneo ya mijini kama SHIVAJINAGAR, MG ROAD, BRIGADE ROAD, kwani uchunguzi wa police bado unaendela na kama tujuavyo India yanapojitokeza mambo kama haya inakuwa ni hatari kwa yeyote Yule atakayekutwa anashangaa shangaa hovyo bila kuwa na mwelekeo.
Barabara nyingi zimekuwa blocked kama ya SAJAPURA,RICHMOND CICLE NA ILE INAYOELEKEA ST MARKS ROAD,RESIDENCY ROAD,MADIWALA,NA PIA INAYOPANDINA JUU BRIGADE ROAD,kwa hiyo traffic jam ni kubwa kwa sasa hapa mjini.

nawaomba mtulie majumbani,message zimetumwa kwa simu lakini ni muhimu pia kupeana habari kwa njia kama hizi za mitandano mbambali,yawezekana wengi wetu tukapitia katika mitandano hiyo nakujua hali ilivyo Bangalore kwa sasa.

pia mitandao ya simu kwa sasa itakuwa inapatikana kwa shida ama kutopatikana kabisa katika kipindi hiki cha milipuko,tunashukuru m/mungu mpaka sasa hakuna mtanzania aliyedhurika mpaka muda huu,nawaomba kwa message zinazotembea ukipata mtumie na mtanzania mwenzako,huku ndiko kuishi kama ndugu kwa sisi waTanzania.

Wale wote mtakao pata taarifa hizii wajulisheni wazazi wenu kwamba mko salama na mnaendelea na shule kama kawaida mpaka muda huu matukio yanatokea,kwani ulinzi umeimarishwa kila kona ya pembe ya Bangalore.

Nawatakia waTanzania wote wa Bangalore kila la kheri katika kipindi kigumu hapa Bangalore,cha msingi ni kukaa majumbani,nikiwa natoa taarifa hii nipokea simu kutoka kwa Evans Makundi wako CHENNAMA CIRCLE karibia na majestic kuna bomu lingine limelipuka Majestic karibia na Bus stand,na police wamelizunguka na pia ulinzi umeimarishwa pale na hivyo kituo cha weza kusimama kwa muda.
Baraka Abdallah Kange
Rais jumuiya ya wanafunzi waTanznaia,Bangalore,India
Email:barakakange@yahoo.com
+919886933877

No comments: