Friday, July 25, 2008

Rais Kikwete ingilia Kati Mgogoro
Huu-Mbatia
Mwenyekiti wa NCCR James Mbatia (Kulia)akimpoza Mjane MARTHA mara baada ya kumkabidhi Tshs laki moja za kujikimu.
Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi,James Mbatia, akimjulia hali mgonjwa,Mariam Karata (70) kutoka Tanga,aliyelazwa kwenye Taasisi ya Moyo jijini Dar es Salaam .
-----
Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kupitia mahakama jijini, iliiamuru Taasisi hiyo kufikia leo kuondoka katika majengo kwa kutolipia pango.Chini ni sehemu ya mapokezi ya taasisi hiyo.
kwa mujibu wa mahojiano na TBC leo uongozi wa nssf umesema umeshafanya kila liwezekanalo kumalizana mwendeshaji wa taasisi hiyo pekee binafsi ya moyo lakini ufumbuzi wa kulipwa hilo pango haujapatikana hata pale suala lilipofika kwa waziri husika.

Akiongea na waandishi muda mfupi kabla ya kutembelea wagonjwa waliolazwa hapo,Mbatia alimuomba Kikwete aingilie kati sakata hili kwa kudai kwamba taasisi hiyo ni nyeti kiasi na haifai iachwe inataabika kwa jinsi inavyosaidia wenye kipato cha chini kupata matibabu ya moyo wakiwa nchini.Picha na Mdau Msimbe na Rwebangira.

No comments: