Thursday, July 24, 2008

libeneke la samaki nchanga mtwara...
wadau wakijichana hapohapo dukani baada ya uzalendo wa kusubiri hadi homu kuwashinda. hakuna zawadi kwa mzalendo atakayeweza kukisia kwa usahihi uhondo wa samaki nchanga..

Picha ya kwanza ni mafungu ya panya yakiuzwa yakiwa ndani yandoo.
Picha ya pili Mama akiwa ameshika mafungu yake baada yakuwanunua kwa kitoweo.

Brother Kadidi.

Hivi karibuni nilitembelea Lukuledi wilayani Masasi mkoani Mtwara. Nikakuta wenyeji wa huko bado wanakula Panya na wanawapenda sana tu.

Nilipowauliza kama ni kwa sababu ya ukosefu wa nyama zingine,walisema Hapana, nyama zingine ikiwemo ya ng’ombe ni nyingi. Ila wanakula panyakwa ajili ya HAMU TU.

Siku hizi panya hawa hawaitwi tena “Yeila” au “Atoro”, baliwanaitwa MKANDA NJE kutokana na kambainayofungwa katika kila fungu ndio wanaifananinsha na mkanda.

Fungu moja linauzwa shilingi 200/= na kila fungu lina panya watano. Ifahamike wazi kuwa panya hawa wanaoliwa sio wale wanaokaa ndani ya nyumba bali hawa huchimba mashimo porini na hukaa huko maporini kwenye mashimo yao.
Yaani hawa ni panya mwitu a.k.a 'samaki nchanga'

Mdau
Perez.
mdau perez!
asante perez kwa nyuzzz hizi na picha. mie mwenyewe mate yananitoka. naendelea kukaribisha wadau kutuletea vitu kama hivi na vinginevyo toka kila pembe ya dunia isomwapo globu hii ya jamii. tuma kupitia safari2e@yahoo.com msisahau salamu, nondozz na kadhalika....

No comments: